Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE K.n.y. MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawawezesha wananchi wa Jimbo la Tarime Vijijini, Tarime Mjini na Rorya kupata bidhaa kutoka nchi jirani ya Kenya?

Supplementary Question 1

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, Wilaya ya Rory ana Tarime moja ya faida ambayo tunaipata kuwepo mpakani kati ya Tanzania na Kenya ni pamoja na unafuu wa bei ya bidhaa ambazo zinazalishwa maeneo ya mpakani.

Swali la msingi hapa lilikuwa linauliza Wizara haioni kuna umuhimu sasa wa kuwasaidia wale wachuuzi wadogo ambao unakuta bidhaa chache, kwa mfano mifuko miwili ya cement, mifuko mitano ya sukari ambayo wakikamatwa wakati mwingine hupewa kesi za uhujumu uchumi au hunyang’anywa pikipiki zao au kutaifishwa bidhaa zao zile chache. Mheshimiwa Waziri haoni kuna umuhimu wa kuwasaidia hawa wafanyabiashara wadogo ili kutengeneza mazingira rafiki angalau waweze kufanya biashara hizi bila usumbufu wanaopata?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili Wilaya ya Rorya tayari tuna eneo ambalo tumelitenga kwa ajili ya kuweka viwanda kwa mahitaji na muktadha wa bidhaa hizo hizo ambazo wananchi wetu wanavuka kwenda kuzifata Kenya.

Je, Wizara ina mpango gani wa kuhakikisha angalau inazungumza na wawekezaji wa bidhaa hizi hizi wanazozalisha Kenya kujenga kiwanda, kuja kuwekeza maeneo ya Rorya ili tuwasaidie hawa wananchi wanaovuka maeneo ya mpaka kwenda nchini Kenya? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Chege kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli moja ya mikakati ambayo tunayo Serikali ni kuona namna gani tunawasaidia wachuuzi au wafanyabiashara wadogo wadogo, wajasiriamali katika mikoa ya mipakani ambao wanafanya biashara kati ya nchi na nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya maelekezo ambayo tulishawaelekeza maafisa wetu wa taasisi zote zinazohudumia wafanyabiashara mipakani ikiwemo TRA, TBS na nyingine kuhakikisha kwanza wanatoa elimu kwa wachuuzi hawa wajasiriamali namna ya kufanya biashara kati ya nchi moja na nyingine. Lakini zaidi waendelee kuwasaidia kwa maana ya kuwapa muda fulani kama angalizo wakati wanaendelea kujifunza namna ya kufanya biashara kati ya nchi hizi mbili.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala la pili nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba moja ya mikakati yenu ni kuona tunawavutia wawekezaji katika kujenga viwanda maeneo ya mipakani ikiwemo katika eneo la Rorya. Kwa hiyo, hilo tutalifanya na tutachukua kwa uzito mkubwa nimwakikishie Mbunge tutalifanya hilo tutashirikiana naye, nitawasiliana naye baada ya kikao hiki. Nakushukuru sana.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE K.n.y. MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawawezesha wananchi wa Jimbo la Tarime Vijijini, Tarime Mjini na Rorya kupata bidhaa kutoka nchi jirani ya Kenya?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru; ni kweli kumekuwa na kero kubwa sana kwa hawa wafanyabiashara wadogo wanaokutwa wanafata bidhaa upande wa pili Kenya. Ni kwa nini sasa Serikali isielekeze task force iache huu utaratibu wa kufukuzana na hawa wafanyabiashara wadogo ambapo wakati mwingine inapelekea vifo kwa kuwagonga ili kuwepo na utaratibu wa kiofisi kama mtu amekwepa kodi basi anafatiliwa kuliko wanavyofanya sasa hivi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali yetu ya Awamu ya Sita chini ya Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan imeshasema na tumeshaelekeza kwamba tuwahudumie wafanyabiashara na hasa tukiwa na lengo la kujenga sekta binafsi yenye nguvu kuhakikisha kwamba wanafanya biashara zao vizuri bila kero. Kwa hiyo, nilichukue hili ili tuone kama kweli shughuli hizo zinafanyika, kero hizo au task force hizo ziweze kukomeshwa mara moja kuhakikisha wanawasaidia badala ya kuwa-harass wafanyabiashara.