Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 7 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 110 2022-09-21

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE K.n.y. MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawawezesha wananchi wa Jimbo la Tarime Vijijini, Tarime Mjini na Rorya kupata bidhaa kutoka nchi jirani ya Kenya?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwita Mwikwabe Waitara, Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania ni miongoni mwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na inatekeleza makubaliano ya hatua ya pili ya ushirikiano ya Soko la Pamoja ambapo wafanyabiashara kutoka nchi wanachama wameruhusiwa kusafirisha bidhaa kutoka nchi moja kwenda nchi nyingine kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa katika nchi husika. Hivyo, kutokana na mazingira hayo, Serikali haijaweka zuio lolote la bidhaa kutoka nchi jirani ya Kenya kuingia Tanzania. Nakushukuru sana.