Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Wapimaji wa Ardhi katika Mji wa Tukuyu Wilayani Rungwe ili kupunguza migogoro ya ardhi?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, kimsingi ninaishukuru Serikali baada ya kupiga kelele kwa muda mrefu imetuletea Mpima mmoja katika Wilaya ya Rungwe.

Swali langu la kwanza; ni kwa nini msiongeze Mpima mwingine kwa sababu Wilaya ya Rungwe ina vitongoji 502 hivyo uhitaji wa Wapima ni mkubwa sana? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili tuna shughuli inayoendelea katika Wilaya ya Rungwe ya upimaji wa vijiji 11 katika upimaji huo tunashukuru Serikali mmeleta shilingi milioni 500 na inafanya revolving fund kwa wananchi kulipa shilingi 30,000 ili wapimiwe.

Ni kwa nini Serikali msiongeze fedha ili wananchi hawa watoe angalau shilingi 15,000 kuwapunguzia makali katika upimaji wa viwanja hasa kwenye vijiji? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA K.n.y. WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante nipende kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwakagenda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na lile swali dogo la kwanza ambalo linaomba nyongeza ya watumishi katika sekta ya wapima kwa sababu wanaye mmoja. Wizara inalichukua na bado inaendelea kulifanyia kazi na upo uwezekano wa kuongeza maofisa hao kulingana na jinsi tutakavyokuwa tumejijengea uwezo wa ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili kuhusu suala la kuongeza fedha ni kweli kabisa kwamba jambo hili ni muhimu na tumelipokea kwanza kwa uzito wa kutosha ili baadae tukalifanyie kazi na kuona uwezekano wa kupata vyanzo vya fedha kwa ajili ya kuongeza nguvu ingawa hatutarajii wapunguziwe thamani ile wanayolipa sasa kwa sababu nayo vilevile inasaidia kuongeza uharakishwaji wa zoezi hili. Ahsante.