Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 7 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 107 2022-09-21

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka Wapimaji wa Ardhi katika Mji wa Tukuyu Wilayani Rungwe ili kupunguza migogoro ya ardhi?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA K.n.y. WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe ina watalaam wa sekta ya ardhi ambao ni Maafisa Ardhi, Mpima Ardhi na Afisa Ramani ambao wanaendelea na utaratibu wa shughuli za ardhi katika Halmashauri hiyo ikiwemo kushughulikia mgogoro wa ardhi. Aidha, Mkoa wa Mbeya una timu ya wapima ardhi ambayo kukiwa na uhitaji wa kupima eneo katika Halmashauri za Mkoa wa Mbeya timu hiyo hushiriki katika kazi za kupima katika maeneo husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara kupitia Ofisi ya Ardhi Mkoa wa Mbeya itapeleka timu ya wataalam wa ardhi katika Wilaya ya Rungwe tarehe 26 Septemba, 2022 ili kushughulikia kero na mgogoro wa ardhi.