Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO K.n.y. MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, ni lini Shirika la Nyumba la Taifa litaanza ujenzi wa Safari City nje kidogo ya Jiji la Arusha?

Supplementary Question 1

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kule Mkoani Mbeya Wilayani Rungwe maarufu kama Tukuyu hakuna Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi yapata miaka minne sasa ambapo Halmashauri ya Busekelo inategemea hapo na tatizo hilo Mbarali kuna tatizo hakuna pia Mwenyekiti na Chunya, ukizingatia wananchi wa Chunya wanatoka mbali kabisa Kambi Katoto wanakwenda Mbeya Mjini ambapo ni karibu na Mkoa wa Tabora. (Makofi)

Sasa je, Serikali ni lini itatupelekea Wenyeviti Baraza la Ardhi kwenye Wilaya hizo? Ahsante. (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi Wizara inaendelea na utaratibu, ni maeneo mengi hayana Mabaraza haya, kwa hiyo Wizara inaendelea kufanya matayarisho kwa ajili ya kuajiri Wenyeviti wa Mabaraza na moja ya watakaoajiriwa tuta-consider hilo eneo la Tukuyu, ahsante. (Makofi)

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO K.n.y. MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, ni lini Shirika la Nyumba la Taifa litaanza ujenzi wa Safari City nje kidogo ya Jiji la Arusha?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo kama Njombe ambayo ni Miji inayokua inauhitaji mkubwa sana wa makazi kwa sasa na maofisi. Ni lini, Shirika la Nyumba litakwenda kuanza mpango wa kujenga nyumba katika maeneo hayo ya Njombe?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kujibu swali la Mheshimiwa Deo, Mbunge wa Njombe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi National Housing inafanya mabadiliko makubwa sana ambayo yanakwenda kuanzisha ujenzi katika maeneo mengi sana ya nchi na hasa pembezoni mwa miji ambayo kwa kweli ilikuwa imesahaulika. Nikuombe tu Mheshimiwa Mbunge kwenye eneo lako hilo muweze kuandaa maeneo ambayo shirika litakapofika lipate ushirikiano wa kupata maeneo ya kujenga nyumba, ahsante.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO K.n.y. MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, ni lini Shirika la Nyumba la Taifa litaanza ujenzi wa Safari City nje kidogo ya Jiji la Arusha?

Supplementary Question 3

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, Shirika la Nyumba lina nyumba nyingi ambazo ni chakavu na ukarabati wake umekuwa ni changamoto kubwa sana hususani kwenye Mkoa wa Tabora hasa Manispaa ya Tabora.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haioni sasa umefika wakati wa kukarabati nyumba hizi na kama wameshindwa basi waziuze? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, nipende kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Tabora, Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi ukarabati unaendelea nchi nzima na kwa sababu hawawezi kufanya vitu vyote kwa pamoja, ndio maana unaona kama Tabora wamechelewa kidogo. Hatuna mpango wa kuuza nyumba zile kwa sababu zinaendelea kuwasaidia watumishi mbalimbali ambao wanazitumia kwa ajili ya kupunguza ile uwezekano wa kukosa nyumba katika maeneo ambayo wanakwenda.

Kwa hiyo, nipende tu kusema kwamba ukarabati unaendelea nchi nzima na muda mfupi ujao mtafikiwa Tabora, ahsante.