Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 7 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 106 2022-09-21

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO K.n.y. MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: -

Je, ni lini Shirika la Nyumba la Taifa litaanza ujenzi wa Safari City nje kidogo ya Jiji la Arusha?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA K.n.y. WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Arumeru kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa Safari City una jumla ya viwanja 1,713 kwa ajili ya uendelezaji wa nyumba na makazi, majengo ya biashara, maeneo ya viwanda vidogo vidogo, huduma za jamii kama shule, hospitali, maeneo ya kuabudia, sehemu za michezo, sehemu za mapumziko na maeneo ya usalama wa mji kama kituo cha polisi na zimamoto pamoja na maeneo ya wazi. Kwa kipindi cha kuanzia Juni, 2022 hadi sasa jumla ya viwanja 970 vyenye thamani ya shilingi bilioni 19.64 vimeuzwa ambapo Shirika la Nyumba la Taifa limekusanya shilingi bilioni 12.33 sawa na asilimia 62.78 ya mauzo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa mradi wa Safari City tayari umeanza ambapo mamlaka zinazohusika zinaendelea na uwekaji wa miundombinu muhimu ya barabara, maji na umeme. Pia Shirika la Nyumba la Taifa tayari limejenga nyumba 10 za gharama nafuu za mfano kuwawezesha wanunuzi wa viwanja takribani 23 kuanza ujenzi ambapo baadhi yao tayari wamehamia katika makazi yao.

Aidha, baadhi ya taasisi za Serikali ikiwemo Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Arusha (AUWSA) na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Ufundi Stadi (NACTVE) zinaendelea na ujenzi katika eneo la mradi. Vilevile Taasisi nyingine ni pamoja na LATRA, OSHA na EWURA zimekamilisha ununuzi wa viwanja na zinatarajia kuanza uendelezaji katika viwanja vyao.