Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: - Je ni lini, Serikali itamaliza mgogoro wa ardhi kati ya vijiji vya Vikonge na Nomalusambo dhidi ya TFS?

Supplementary Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa Msitu wa Mpanda North East ulishapoteza hadhi ya uhifadhi kutokana na shughuli za kibinadamu, pamoja na Serikali yenyewe kuchangia kwa kugawa maeneo kuyafanyia shughuli za maendeleo ukiwemo Mji wa Mpanda pale Mpanda Mjini ni eneo la TFS, makazi ya Katumba na vijiji vilivyotajwa.

Je, ni lini Serikali itakuja kutatua huo mgogoro kumaliza mgogoro huo kwa kupitia timu ya Mawaziri wanane ambao Serikali ilielekeza?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa TFS imekuwa na tabia ya kuwapiga wananchi, kuwaibia mali zao kila wanapozalisha mali, kipindi cha uzalishaji mali hawaendi kuwapiga na kipindi cha uvunaji wanakwenda kuwanyang’anya mali zao. Ni lini tabia hii itakomeshwa? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kakoso, Mbunge wa Mpanda Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba pamoja na majibu ya msingi maeneo haya yaliingizwa kwenye timu ya Mawaziri wa kisekta nane ambao walikwenda kuchakata na pia wameweza kufika katika mikoa 13 kutoa maelekezo ya namna ya kutatua changamoto hizi za migogoro. Hivi ninavyoongea sasa kuna wataalam wako katika maeneo hayo ikiwemo Mpanda Vijijini ambako wataalam wamekwenda kufanya tathmini hiyo. Maeneo haya kama kweli yanakosa sifa ya kuwa hifadhi basi yataingizwa kwenye utatuzi wa migogoro ya Mawaziri nane na kisha yataingizwa kwenye ufutaji wa GN ambazo zipo tangu mwaka 1947.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye upande wa TFS kunyang’anya mazao, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kama kuna changamoto ya namna hii ambayo imejitokeza, basi naomba nilichukue, twende kulifanyia kazi na wananchi waweze kuendelea na shughuli zao za kila siku. Ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: - Je ni lini, Serikali itamaliza mgogoro wa ardhi kati ya vijiji vya Vikonge na Nomalusambo dhidi ya TFS?

Supplementary Question 2

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kunipa nafasi hii.

Kwa kuwa na sisi katika Kijiji cha Luhimbalilo, Kata ya Mputa, Wilaya ya Namtumbo kumekuwa na fukuto la mgogoro kati ya TFS na kijiji hicho kuhusiana na hifadhi ya Matogolo kuingilia eneo la Kijiji cha Luhimbalilo.

Je, Serikali inaweza kuelekeza sasa kikosi cha wataalam wakaja kufanya mazungumzo na kutafsiri hiyo mipaka ili kuondosha mgogoro huo? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Namtumbo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe tu kwamba migogoro yote ambayo inatuletea changamoto katika uhifadhi niwaombe Waheshimiwa Wabunge tuipokee ili tuweze kuleta wataalam waweze kufafanua mipaka na pale ambapo pana uhitaji wa namna ya kuachia maeneo kwenye maeneo ambayo yamevamiwa zaidi tutakaa chini, tufanye tathmini na kisha tuondokane na hii migogoro ya kila siku ili maeneo ambayo tumeyahifadhi basi yaendelee kuhifadhiwa vizuri kwa maslahi ya Taifa letu.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: - Je ni lini, Serikali itamaliza mgogoro wa ardhi kati ya vijiji vya Vikonge na Nomalusambo dhidi ya TFS?

Supplementary Question 3

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Waziri mlikuja kwenye Kijiji cha Handa Kata ya Lahoda pamoja na timu ya Mawaziri watano na wewe ukiwemo mlikutana na changamoto kubwa sana, kuhusiana na Hifadhi ya Swagaswaga na wananchi walieleza changamoto wanayoipata kutokana na hifadhi hiyo na mkaunda timu ya wataalam kwa ajili ya Kwenda kutafsiri mipaka.

Je, ni lini Serikali itakwenda kuwaeleza wananchi tafsiri ya mipaka hiyo kwa sababu bado wananchi wale wanapigwa, bado wananchi wale wananyang’anywa mazao yao, wanadhalilishwa; nataka kujua ni lini mtakwenda kutoa hayo majibu kwa wananchi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kunti, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya wataalam kufika katika maeneo hayo na kufanya tathmini niwaombe wananchi waendelee kusubiri maamuzi ya Serikali, wasiendelee kuvamia maeneo hayo na kujichukulia mamlaka ya kwamba tayari tumeyaachia. Ni mpaka pale Serikali itakapotoa tamko kwamba sasa tunaachia eneo hili, basi wananchi waendelee kufanya shughuli hizo.

Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge wasubiri kuwa tunachakata tutayaleta majibu.