Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 7 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 104 2022-09-21

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: -

Je ni lini, Serikali itamaliza mgogoro wa ardhi kati ya vijiji vya Vikonge na Nomalusambo dhidi ya TFS?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Moshi Selemani Kakoso, Mbunge wa Mpanda Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mgogoro wa ardhi uliokuwepo kati ya Hifadhi ya Msitu wa Mpanda North East na Kijiji cha Vikonge ulitokana na kutotambulika mipaka. Wizara kwa kushirikiana na Serikali za Vijiji, wananchi pamoja na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi walienda kutafsiri mipaka hiyo. Hivyo, Serikali inahimiza kuendelea kuheshimu makubaliano yaliyosainiwa kati ya Kijiji cha Vikonge na TFS juu ya mpaka na hivyo kumaliza mgogoro huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Kijiji cha Nomalusambo ambacho kina kitongoji kiitwacho Ijenje ambacho kiko ndani ya Hifadhi ya Msitu wa Mpanda North East, mwaka 2017 kitongoji hiki kiliondolewa katika eneo la hifadhi kupitia zoezi la uondoaji wavamizi msituni ambapo wananchi wa kitongoji hicho walitii maekelezo na kuondoka ndani ya hifadhi. Hivyo, Serikali inashauri wananchi wa Kijiji cha Nomalusambo waendelee kushirikiana na Serikali katika kuhifadhi Hifadhi ya Msitu wa Mpanda North East kwa ajili ya manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo. (Makofi)