Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Kolandoto - Mhunze hadi Mwangongo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina swali moja la nyongeza.

Swali hili ni kuhusiana na habari ya shilingi bilioni moja ambayo imetengwa. Unaweza kuona ni kiasi kidogo sana cha fedha, nilitaka nipate majibu na wananchi wa Jimbo la Kishapu wapate majibu kwamba kiasi hiki cha fedha tafsiri yake ni nini kwa sababu bilioni moja ni kiasi kidogo sana ili na matumini wawe wananchi wa Kishapu? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Boniphace Nyangindu Butondo, Mbunge wa Kishapu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kwa ukubwa wa barabara hii, hii fedha ambayo imetengwa haiwezi kuikamilisha, lakini nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge ni utaratibu kwamba barabara hizi hazijengwi kwa siku moja wala kwa mwaka mmoja na ndiyo maana mpango ambao tunautumia kwa kujenga barabara ni ku-raise certificate. Kwa hiyo, wakishaanza kila watakapokuwa wamefika hatua nyingine wanaandika certificate, wanalipwa na ndiyo utaratibu ambayo tumekuwa nao katika ujenzi wa barabara zetu baada kazi ana-raise certificate na Serikali inalipa hizo fedha. Kwa hiyo, ni barabara kuu tunalijua hilo na ndiyo maana tayari tumeanza kuandaa taratibu za kutangaza hiyo barabara. Ahsante. (Makofi)

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Kolandoto - Mhunze hadi Mwangongo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mbuyu wa Mjerumani kupitia Magala hadi Mbulu kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Mbuyu wa Mjerumani kwenda Mbulu ni barabara ambayo ndiyo tumekamilisha usanifu wa kina ikiwa ni maandalizi kwa kuijenga kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge ipo kwenye mpango, tulichokuwa tunafanya ni kukamilisha usanifu na tukishakamilisha Serikali itaendelea kutafuta fedha ili kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Kolandoto - Mhunze hadi Mwangongo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Nakumbushia barabara ya kutoka Kibaoni – Mfinga inapita Mto Wisa inakuja kutokea Mloo, barabara hii ni muhimu sana kwa Mkoa wa Rukwa.

Je, ni lini itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba nikubaliane na Mheshimiwa Bupe Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa kwamba barabara aliyoitaja inaunganisha Mkoa wa Mbeya na Rukwa hadi Katavi, ni barabara ambayo tayari upande mwingine imeshakamilika usanifu lakini bado tunaendelea kukamilisha usanifu wa kina kwa kipande kingine tayari tumeshaanza kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Kolandoto - Mhunze hadi Mwangongo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, ni lini Serikali itaendeleza ujenzi wa barabara ya lami iliyoishia katika Kijiji cha Elelai kuelekea Kamwanga inayounganisha Wilaya ya Longido na Wilaya ya Siha inayozunguka Mlima Kilimanjaro?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE):
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Magige, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja ni barabara muhimu sana iko kule mpakani. Baadhi ya sehemu tumeshaikamilisha na sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha ili iweze kuiunganisha barabara yote kwa lami na iweze kupitika kwa urahisi. Ahsante.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Kolandoto - Mhunze hadi Mwangongo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. IDDI KASSIM IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara inayotoka Solwa kuja Moktolio – Bulige - Ngaya mpaka Kahama ni barabara iliyoko kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi na inatakiwa ijengwe kwa muda mrefu sasa. Sasa swali langu ni lini fedha hizi zitatengwa ili barabara hii ianze ujenzi mara moja? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi Kassim, Mbunge wa Msalala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara niliyoitaja ipo kwenye mpango na ipo kwenye Ilani, kwa hiyo, Serikali inaendelea kutafuta fedha ili ijenge kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Kolandoto - Mhunze hadi Mwangongo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi; nataka nijue ni lini ujenzi wa barabara wa Mbande - Kisewe - Msongola utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii itaanza kujengwa kama tulivyoipanga kwenye bajeti ya mwaka huu wa fedha.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Kolandoto - Mhunze hadi Mwangongo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru; barabara ya Bugene – Itela - Nkwenda mpaka Kaisho ambazo ni ahadi ya Mheshimiwa Hayati Rais Magufuli, kilometa 50. Ni lini barabara hii itaanza kujengwa? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni ahadi ya Mheshimiwa Rais, Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kutimiza hiyo ahadi.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Kolandoto - Mhunze hadi Mwangongo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, tumepata barabara ya mchepuo ya kilometa tatu ambapo mvua ikinyesha hali itakuwa mbaya zaidi. Je, Serikali ni lini itatujengea barabara ya lami kwa maeneo hayo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Fyandomo, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Mbeya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, hiyo barabara tuliyojenga ni kwa ajili ya dharura ili kuepusha ajali zilizokuwa zinatokea. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mpango wa Serikali sasa ni kuijenga barabara hiyo ya lami. Kwa hiyo, Serikali inatafuta fedha ili iijenge na liwe ni suluhisho la kudumu. Ahsante. (Makofi)