Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 103 2022-09-21

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: -

Je, ni lini barabara ya Kolandoto - Mhunze hadi Mwangongo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Nyangindu Butondo, Mbunge wa Kishapu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilishakamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Kolandoto – Mhunze hadi Mwangongo (kilometa 53) kwa lengo la kuijenga kwa kiwango cha lami. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi bilioni moja kwa ajili ya kuanza maandalizi ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Zabuni kwa ajili ya kazi hiyo zitatangazwa mwezi Novemba, 2022. Ahsante. (Makofi)