Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, Serikali ina mikakati gani kuelimisha wananchi wanaozunguka Hifadhi za Misitu kuhusu biashara ya uuzaji/utunzaji wa hewa ukaa?

Supplementary Question 1

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; je, katika kuandaa mwongozo huo TFS ambao wamekuwa na migogoro na wananchi wanaozunguka hifadhi hizo za misitu wameshirikije?

Swali la pili; je, Serikali haioni haja ya kushuka kwa wananchi na kutoa elimu ya biashara ya hewa ya ukaa ili kujenga ufahamu zaidi? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA
MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felix, Mbunge wa Buhigwe, najibu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba moja miongoni mwa wadau ambao watakuwa ni sehemu kubwa ya mwongozo huo ni TFS na nimwambie kwamba tumewashirikisha vya kutosha katika mwongozo huu na siyo wao tu; tumeshirikisha taasisi nyingi za kibinafsi na za Serikali, lakini zaidi tumewashirikisha sana Tawala za Mikoa wakiwemo Halmashauri, Majiji, Wilaya, Mikoa na Vijiji ili lengo na madhumuni na wao wawemo katika sehemu ya mradi huo ili watusaidie katika kuwaeleza wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa kuwafikishia taaluma wananchi, hili jambo ni la mwanzo tumelipa kipaumbele na tayari timu ipo imeelezwa katika mpango huo, kutakuwa na timu maalum ambayo itapita nchi nzima kuzunguka kwa ajili ya kutoa kwanza elimu kwa wananchi wafahamu mradi huo na faida zake, lakini wafahamu fursa zinazopatikana katika mradi huo, lakini wafahamu faida za kimazingira ambazo zitapatikana katika mradi huu. Nakushukuru.