Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 7 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 100 2022-09-21

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: -

Je, Serikali ina mikakati gani kuelimisha wananchi wanaozunguka Hifadhi za Misitu kuhusu biashara ya uuzaji/utunzaji wa hewa ukaa?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Maziringira, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kavejuru Eliadory Felix, Mbunge wa Buhigwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha kuwa Watanzania na Serikali inanufaika na biashara ya hewa ukaa. Serikali Kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na Wizara za kisekta pamoja na wadau inaandaa mwongozo na kanuni za usimamizi wa biashara ya hewa ukaa ambazo zinatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Oktoba, 2022. Mwongozo na kanuni hizo zitaonesha namna ya utaratibu na kusimamia biashara hiyo ikiwemo mgawanyo wa manufaa kwa wadau watakaohusika katika mnyororo wa biashara ya hewa ukaa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, baada ya kukamilika kwa mwongozo na kanuni, Serikali imejipanga kuendelea kutoa elimu kuhusu biashara ya hewa ukaa kwa wadau mbalimbali wakiwemo wananchi ambao ni sehemu kubwa ya biashara hiyo inayofanyika katika maeneo yao. Nakushukuru.