Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza: - Je, ni lini Sheria ya Manunuzi na Ukandarasi kupitia Public Private Partnership itaanza kutumika?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu ya Serikali, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; kwa kuwa kwa mujibu wa Sheria hii ya PPP kwa maana ya Sheria Sura namba 210, kiwango cha mtaji kwa wazawa ni dola milioni 20. Je, Serikali haioni kwamba kiwango hiki ni sehemu ya kikwazo cha utekelezaji wa sheria hii?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Serikali ina mpango gani wa kupunguza masharti ya kimkataba katika miradi hii inayoibuliwa na sekta binafsi ili iweze kutekelezwa kwa ufanisi kupitia PPP? Ahsante.

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sheria ya PPP ipo katika mchakato wa kufanyiwa marekebisho na sasa ipo ngazi ya kukusanya maoni kutoka kwa wadau. Kwa hiyo nimwombe Mheshimiwa Mbunge awe na subira mpaka mchakato huo utakapokamilika bila shaka hiki hakitokuwa kikwazo kwa utekelezaji wa sheria hiyo.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, masharti hayo ambayo yapo pia ni kwa mujibu wa sheria na taratibu, kwa hiyo pia nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge masharti hayo huenda yakapungua baada ya kupata mapendekezo kutoka kwa wataalam wetu ambao wanakusanya maoni hayo. Ahsante.