Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 8 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 130 2022-09-22

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza: -

Je, ni lini Sheria ya Manunuzi na Ukandarasi kupitia Public Private Partnership itaanza kutumika?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura 410 ipo na inatumika, sambamba na Sheria ya PPP, Sura 210, ambapo mchakato wa zabuni za miradi ya PPP unazingatia sheria zote mbili. Pamoja na sheria hizo kutumika kama rejea wakati wa ununuzi wa miradi ya ubia, Serikali inaendelea na utaratibu wa kupokea maoni na mapendekezo kutoka kwa wadau ili kurekebisha vifungu vyenye changamoto katika utekelezaji wake. Ni matarajio yetu kwamba, marekebisho ya sheria zote mbili yatakamilika katika mwaka 2022/2023. Ahsante.