Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE K.n.y. MHE. REUBEN N. KWAGILWA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme mitaa 28 ya Jimbo la Handeni Mjini ambayo bado haijapata umeme?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; je, ni lini Serikali itajenga kituo cha kupozea umeme pale kwa Mbwembwele ili kuondosha tatizo la kukatikakatika katika Mji wa Handeni?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; mkandarasi anayesambaza umeme wa REA katika Wilaya ya Korogwe, anafanya kazi kwa kusuasua, tangu mkataba ulipoanza mwezi Mei, amesimamisha nguzo katika vijiji vitatu tu. Je, ni nini kauli ya Serikali kuhusiana na mkandarasi huyu? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza yaliyoulizwa na Mheshimiwa Ulenge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la kwanza Serikali tayari imetoa pesa, shilingi bilioni 500 kwa ajili ya kuimarisha mfumo wa grid ya Taifa na Wilaya ya Handeni ni mojawapo ya eneo ambapo patajengwa kituo cha kupooza umeme katika eneo la Mkata kwa kuanzia na kinajengwa mwaka huu wa fedha wa 2022/2023.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la pili, mkandarasi anayepeleka umeme vijijini katika eneo la Korogwe, tutahakikisha kwamba kufikia Desemba mwaka huu anakamilisha kazi kwa sababu ndiyo mujibu wa mkataba. Tunaendelea pia kufuatilia kwa karibu kuondoa zile changamoto ndogo ndogo ambazo zilikuwa zimejitokeza za upungufu na ukosefu wa vifaa lakini kazi zitakamilika kwa wakati.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE K.n.y. MHE. REUBEN N. KWAGILWA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme mitaa 28 ya Jimbo la Handeni Mjini ambayo bado haijapata umeme?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante, je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika vitongoji 42 vilivyobakia katika Jimbo la Kalenga, Mkoani Iringa?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, Iringa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kupeleka umeme katika vitongoji vyote nchini kwa jinsi upatikanaji wa fedha unavyoendelea. Hatua ambayo tunaendelea nayo sasa ambayo inatakiwa kukamilika ni hatua ya vijiji ambayo itakamilika Desemba mwaka huu na fedha zinavyozidi kupatikana, vitongoji vinapelekewa pia umeme.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE K.n.y. MHE. REUBEN N. KWAGILWA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme mitaa 28 ya Jimbo la Handeni Mjini ambayo bado haijapata umeme?

Supplementary Question 3

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme katika vijiji vya Kata ya Kiru na Magara, Jimbo la Babati Vijijini?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia Halamga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, umeme vijijini katika eneo alilolitaja utakamilika mwezi Desemba, Mkandarasi wa Giza Cable Industries Limited ambaye anapeleka umeme katika Mkoa wa Manyara, anaendelea na kazi na tutaendelea kusukumana naye ili akamilishe kazi kwa wakati.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE K.n.y. MHE. REUBEN N. KWAGILWA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme mitaa 28 ya Jimbo la Handeni Mjini ambayo bado haijapata umeme?

Supplementary Question 4

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, mkandarasi anayepeleka umeme Kibaha Vijijini kwenye Kijiji cha Kimaramisale, tulikubaliana afike site kwa maelezo yake mwezi wa Sita na mpaka sasa hajafika. Je, ni nini kauli ya Serikali kwa mkandarasi huyu ili akamalizie kazi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Michael, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, wakandarasi wote wa REA wako katika maeneo yao ya kazi mbalimbali. Unakuta mkandarasi mmoja katika mkoa mmoja labda ana wilaya nne au tano na tulipunguza kazi. Naomba nieleze kwamba baada ya hapa nitalifuatilia jambo hili kujua kwa nini mkandarasi huyu hajafika na kama amefika maeneo mengine basi ni lini atafika katika eneo la Mheshimiwa Mbunge alilouliza.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE K.n.y. MHE. REUBEN N. KWAGILWA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme mitaa 28 ya Jimbo la Handeni Mjini ambayo bado haijapata umeme?

Supplementary Question 5

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Kitongoji cha Ngana katika Wilaya ya Rungwe kina kaya 600, lakini waliowekewa umeme wa REA ni kaya 32 peke yake. Serikali haioni interval ni kubwa sana na ni lini itaweza kupeleka umeme katika eneo lile?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maendeleo ni hatua na nia ya Serikali ni kuhakikisha kila mwananchi mahali popote alipo anafikiwa na umeme. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali inaendelea kupeleka umeme kwenye maeneo ya vijiji na vitongoji na kila mwananchi atafikiwa kulingana na upatikanaji wa fedha.