Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 120 2022-09-22

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE K.n.y. MHE. REUBEN N. KWAGILWA
aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme mitaa 28 ya Jimbo la Handeni Mjini ambayo bado haijapata umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Reuben Nhamanilo Kwagilwa, Mbunge wa Handeni Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Handeni Mjini lina jumla ya mitaa 60. Kati ya mitaa hiyo 32 ina umeme sawa na asilimia 53.3 na mitaa 28 haina umeme sawa asilimia 46.7.

Mheshimiwa Spika, Mitaa yote 28 ya Handeni Mjini ipo katika mpango wa kupatiwa umeme kupitia Mradi wa Umeme Vijijini, awamu ya tatu, mzunguko wa pili, unaotekelezwa na mkandarasi kampuni ya Derm Electrics Tanzania ambaye yupo eneo la kazi na anaendelea na ujenzi wa miundombinu ya umeme katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Handeni.

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi huu utakamilika Mwezi Desemba, 2022.