Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuufanya Uwanja wa KIA kutumika kuinua kilimo na kuruhusu ndege za mizigo kutua bila kulipa Landing Fees?

Supplementary Question 1

MHE. SAASISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, kwanza naipongeza sana Serikali kwa kupokea ushauri na kuanza kuufanyia kazi, lakini naipongeza kwa kununua ndege za mizigo. Swali la kwanza; kwa kuwa sasa Serikali imekubali kupokea ushauri, je, Serikali iko tayari kutangaza Uwanja wa Kimataifa wa KIA kuwa uwanja wa kimkakati wa kusafirisha mazao ya kilimo na mifugo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa tayari Serikali imeshatenga fedha na utaratibu wa kuanza kujenga common use facility ndani ya Jimbo la Hai. Je, Serikali haioni iko haja sasa ya kujenga kiwanda cha kutengeneza maboksi kwa ajili ya kusafirishia bidhaa zinazotokana na mifugo na kilimo?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. FREDY A. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza Mheshimiwa Saasisha Elinikiyo Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia suala hili la ndege za mizigo. Katika maswali yake mawili ya kwanza anasema je, Serikali tuko tayari kutangaza uwanja huu kuwa ni wa kimkakati. Sisi Serikali kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri tunatangaza rasmi uwanja wa KIA kuwa ni uwanja wa kimkakati kwa mazao, hususan maua, matunda, mboga mboga pamoja na nyama pamoja na viwanja vingine kama cha Songwe International Airport kilichopo Mkoani Mbeya pamoja na Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, anataka kufahamu ni kwa namna gani tunaweza tukashirikiana pia na wenzetu Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara katika kukuza eneo hili na kujenga viwanda vidogo.

Mheshimiwa Spika, uwanja wa KIA tayari tumeshatenga hekari ama hekta 711 kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vidogovidogo, lakini pia kwa kushirikiana na wawekezaji na tayari tumeshaanza kufanya hiyo hatua. Ahsante.