Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 119 2022-09-22

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kuufanya Uwanja wa KIA kutumika kuinua kilimo na kuruhusu ndege za mizigo kutua bila kulipa Landing Fees?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saasisha Elinikiyo Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa sasa hakuna ndege mahsusi za mizigo zenye ratiba maalum zinazotua KIA. Mizigo yote inayopitia KIA hubebwa na ndege za abiria kwenye sehemu ya mizigo. Aidha, kwa sasa idadi ya ndege kubwa za abiria imeongezeka na hivyo kuongeza uwezo wa kubeba mizigo.

Mheshimiwa Spika, Serikali inafanya juhudi mbalimbali kuimarisha biashara ya usafirishaji wa mizigo kwa njia ya anga ikiwemo kununua ndege maalum ya mizigo (Boeing 767 – 300F) ambayo inatarajiwa kuingia nchini kufikia Juni, 2023, kwa lengo la kuhakikisha kwamba biashara hiyo inaimarika. Aidha, ili kuvutia biashara ya mizigo, Serikali ipo tayari kufanya mapitio ya landing fee kwa ndege za mizigo kama ilivyopendekezwa na Mheshimiwa Mbunge. Ahsante.