Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawekeza katika Sekta ya Michezo hasa kwenye timu za wanawake ili kuibua vipaji kwa watoto?

Supplementary Question 1

MHE. JANETH E. MAHAWANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa ya kuuliza swali la nyongeza. Swali linasema: Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu mkakati wa muda mrefu wa kuendeleza vipaji vinavyopatikana kutokana na mashindano ya UMITASHUTA na UMISSETA?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Janeth, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Janeth amependa kufahamu kauli ya Serikali kuhusu kuendeleza vipaji vya vijana wetu vinavyotokana na UMISSETA na UMITASHUMTA.

Mheshimiwa Spika, sisi Wizara yetu kwanza tumshukuru tumshukuru Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan, amehakikisha kwamba michezo hii imerudi na ametoa maelekezo kwa Serikali. Tunashirikiana na TAMISEMI, Wizara ya Elimu, pamoja na Wizara yetu, kuhakikisha michezo hii inaendelea, kwa kuwa michezo hii ndiyo inatupatia vipaji vya vijana wetu wanaonzia huko chini kuingia timu za Taifa.

Mheshimiwa Spika, hivi sasa Wizara yetu inaendelea ku-review kiasi cha fedha kinachotengwa kwa ajili ya UMISSETA na UMITASHUMTA ili michezo hii iwe endelevu. Ahsante. (Makofi)