Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 8 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 116 2022-09-22

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawekeza katika Sekta ya Michezo hasa kwenye timu za wanawake ili kuibua vipaji kwa watoto?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Elius Mahawanga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuwekeza katika kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji vya michezo ambapo kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Shilingi milioni 183.5 zimetengwa kama kianzio katika kutoa huduma kwa timu zetu za Taifa ikiwemo timu za wanawake na Shilingi bilioni 10 zimetengwa kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya michezo.

Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali imefanya uwekezaji mkubwa katika Timu za Taifa za wanawake ambapo kupitia uwekezaji huu, timu hizi zimeendelea kufanya vizuri katika ukanda wa CECAFA na COSAFA na umewezesha timu ya Serengeti Girls kufuzu mashindano ya Kombe la Dunia nchini India. Ahsante. (Makofi)