Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza: - Je, ni nini kinachosababisha kesi 1,097 za kodi za muda mrefu zenye thamani ya shilingi trilioni 360 na dola za Marekani milioni 181.4 kutoamuliwa hadi sasa?

Supplementary Question 1

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Taarifa ya CAG ya mwaka 2019/2020 na mwaka 2020/2021 kesi hizo nilizozitaja zimesajiliwa katika Mabaraza yetu; Baraza la Rufani za Kodi (TRAT) na Bodi ya Rufani za Kodi (TRAB) zilisajiliwa kesi hizi zenye thamani ya trilioni 360 na hivyo kama majibu ya Serikali kwamba hakuna kesi ya trilioni 360 wakati kwa mujibu wa Taarifa ya CAG hizi kesi zilikuwa zimesajiliwa na Mabaraza haya; hizi kesi zipo wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, zipo taarifa za uhakika kwamba katika mwaka huu wa fedha Serikali iliamua kupokea shilingi bilioni 700 kupitia katika hizo kesi za shilingi trilioni 360 na katika kipindi cha Disemba, 2021 na Februari, 2022 Serikali ilipokea fedha hizo na kuzifuta kesi zenye thamani ya shilingi trilioni 360. Kwa nini Serikai iliamua kupokea fedha bilioni 700 badala ya shilingi trilioni 360 kama madai halali ya nchi? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa maswali yake aliyoyaleta, lakini naomba niweke kumbukumbu sawa; jambo hili hata jana nimeona limejadiliwa kwa kirefu sana na nitakuomba unipe dakika ili niweze kuliweka sawa.

Mheshimiwa Spika, jambo hili liko namna hii, ni kweli anachosema Taarifa ya CAG ya mwaka 2019 ilisema hivyo na Taarifa ya CAG ya mwaka 2019 maana yake ni ukaguzi wa vitabu vya mwaka 2018 (mwaka unaofuatia nyuma yake) lakini kilichofanyika ni kipi?

Mheshimiwa Spika, baada ya mzozo kujitokeza kati ya kesi ya Acacia pamoja na Serikali, Acacia aliuza jambo lile kwa Barrick na Rais wa wakati ule, Rais Magufuli aliunda timu ya kufanya makubaliano na hawa watu mwaka 2017/2018 na makubaliano hayo yaliendelea kwenye mjadala, yakaisha tarehe 24 Januari, 2020 na sherehe hizi zilifanyika Ikulu mbele ya Rais Magufuli na shamrashamra kubwa na Tanzania tukakubali kuachilia shilingi trilioni 360 tumalize shauri lile na tukaunda Kampuni ya Twiga na nchi nzima tunasheherekea kampuni ile kwamba ina ubia wa asilimia 16 kwa Serikali na asilimia 84 kwa Barrick.

Mheshimiwa Spika, na mambo mengine yaliyokubaliwa kwenye makubaliano hayo la kwanza ni lile la ubia kwamba Serikali tutakuwa na asilimia 16 na wao watabakiza asilimia 84.

La pili, wao walikuwa na kesi na sisi ya dola bilioni 2.7 wakafuta kesi hiyo; la tatu, tukakubaliana kwamba watatoa dola milioni 40 kwa ajili ya ujenzi wa barabara ambayo hata kwenye briefing ndio Mbunge wa Kahama aliyekuwa anaiulizia, tukakubaliana hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, si hilo tu, tukakubaliana kwamba watakuwa wanatoa dola sita kwenye kila wakia ya dhahabu na tukakubaliana kwamba watatoa dola milioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa maabara ya madini.

Kwa hiyo, haya yalikuwa sehemu ya frame work agreement ile ambayo ilikubalika na baada ya hapo tukawa tumeshamaliza yale mashauri yakiwemo na mengine ambayo yaliyokuwa yanahusisha mjadala kwenye makubaliano yale yaliyokuwa yanafanyika.

Mheshimiwa Spika, sasa baada ya kuwa imeshafanyika hivyo, kilichofanyika kingine ilikuwa ni kuanza kupokea gawio baada ya kuwa jambo lile limeshafungwa tangu mwaka 2020, kama lilishafungwa tangu mwaka 2020 kilichofuatia mwaka 2021 tulipokea gawio, mwaka 2022 tumepokea gawio na dola milioni 300 ambazo ndio kama bilioni 700 ilikuwa sehemu ya makubaliano kwenye mjadala uliofanyika na sherehe ile ilifanyika Ikulu, mbele ya Rais Magufuli. (Makofi)