Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 153 2022-09-23

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza: -

Je, ni nini kinachosababisha kesi 1,097 za kodi za muda mrefu zenye thamani ya shilingi trilioni 360 na dola za Marekani milioni 181.4 kutoamuliwa hadi sasa?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Luhaga Joelson Mpina, Mbunge wa Kisesa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali haina kesi 1,097 za kodi za muda mrefu zenye thamani ya shilingi trilioni 360 na dola za Marekani milioni 181.4 ambazo hazijaamuliwa. Aidha, hadi Agosti, 2022 kulikuwa na mashauri 854 kwenye hatua mbalimbali za usikilizaji yenye kodi inayobishaniwa ya jumla ya shilingi 4,207,442,214,759.93 (trilioni 4.21) na dola za Marekani 3,480,867.96 (milioni 3.48) katika Bodi ya Rufaa za Kodi na Baraza la Rufaa za Kodi.

Hivyo, kwa sasa taasisi za rufaa za kodi zinaendelea kusikiliza mashauri hayo pamoja na mashauri mapya yanayoendelea kusajiliwa. Vilevile kwa nyakati tofauti, idadi ya mashauri ya kodi hupungua au kuongezeka kulingana na kasi ya usikilizaji na usajili.