Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarudisha huduma ya treni Manyoni – Singida?

Supplementary Question 1

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, namshukuru sana Naibu Waziri kwa majibu mazuri ambayo yanaleta matumaini kwa wananchi wa Singida kwa kufufua reli hii ya Singida – Manyoni. Pamoja na majibu hayo, ninayo maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kupata commitment ya Serikali, nataka kujua ni fedha kiasi gani zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza mradi huu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa lengo la reli hii lilikuwa ni kukuza uchumi, kubeba mizigo ambayo ipo katika ukanda huu na hasa ililenga sana wakati huo Mwalimu Nyerere akianzisha reli hii ni kubeba ngano ambayo iko kule Basutu katika Mkoa wa Manyara. Sasa kwa sababu tunakuza eneo la kilimo na tuna madini yako pale kwenye Mkoa wa Singida, ni mpango gani wa Serikali sasa kuujenga kwa kiwango cha SGR ili iwe na uwezo mkubwa wa kubeba mizigo katika eneo hilo? Ahsante sana.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Miraji Jumanne Mtaturu, Mbunge wa Singida Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka 2022/2023, tumetenga fedha kiasi cha shilingi bilioni 3.45 kwa ajili ya ukarabati wa tuta pamoja na makalavati na uwekaji wa tabaka la kokoto na tutajenga kama ambavyo tuliboresha reli ya kutoka Tanga kwenda Arusha kupitia Moshi kwa maana ya kutumia force account.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, anapenda kujua ni lini sasa hii reli itakuwa katika kiwango cha standard gauge? Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa kwa jitihada zake pamoja na Waheshimiwa Wabunge wengine wa Mkoa wa Singida, Serikali mara baada ya kufanya ukarabati huu wa awali, tukifungua malango/tukifungua njia, ndipo tutakapoanza sasa kufanya tathmini, feasibility study kwa ajili ya SGR. Ahsante.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarudisha huduma ya treni Manyoni – Singida?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Je, ni lini treni ya mwendokasi itaanza kufanya kazi kati ya Dar es Salaam na Morogoro? Ahsante sana.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, matarajio yetu yalikuwa reli ya SGR kutoka Dar es Salaam kuja Morogoro yenye urefu wa kilometa 300 tulitegemea ingeanza mwezi huu wa Septemba kama ambavyo tulijibu hapo awali wakati wa Bunge la Bajeti. Lakini kutokana na changamoto mbalimbali hususan katika kusafirisha vipuri na mabehewa ambayo kulikuwa kuna changamoto ya kupata meli ya usafirishaji kutoka nchini Ujerumani kuja Tanzania, lakini habari njema kwa Watanzania wote watambue ya kwamba tayari vichwa vya treni, mabehewa ya abiria na mizigo, hivi ninavyosema vimekwishapakiwa kwenye meli kuja nchini Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tunataraji kwamba ifikapo mwezi Novemba, mwaka huu vitakuwa vimeshaingia na tutafanya majaribio mpaka mwezi Januari. Kwa hiyo, mwezi Februari mwakani standard gauge kutoka Dar es Salaam kuja Morogoro itaanza rasmi, ahsante. (Makofi)