Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 141 2022-09-23

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itarudisha huduma ya treni Manyoni – Singida?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Miraji Jumanne Mtaturu, Mbunge wa Singida Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TRC katika bajeti ya mwaka 2022/2023 imetenga fedha kwa ajili ya kufanya tathmini na maadalizi ya awali ya kufufua njia ya Manyoni – Singida yenye urefu wa kilometa 115 ambayo ilifungwa takribani miaka 30 iliyopita. Lengo la kufufua njia hii ni kuboresha usafirishaji wa mizigo na abiria pamoja na kukuza uchumi wa maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC) inaendelea na mchakato wa ununuzi wa wakandarasi watakaofanya tathmini ya mahitaji na maandalizi ya awali ya kutekeleza mradi huo. Ahsante.