Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka CCTV camera na alarm systems katika masoko, shule na sehemu za wazi zenye mkusanyiko?

Supplementary Question 1

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.

Kwa kuwa teknolojia inabadilika kila wakati; je, Serikali imejipanga vipi kuhakikisha kuwa hizo CCTV camera na alarm systems zinahuishwa kila wakati?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Serikali imeshachukua hatua ya kuanza kufunga mifumo ya kutambua na kudhibiti majanga kwa majengo mapya; je, Serikali inatoa kauli gani kwa majengo ya zamani? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Lucy John Sabu, Mbunge wa Viti Maalumu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tumeshaweka mpango wa kitaifa wa kudhibiti majanga hususani majanga ya moto na tayari tumeshaanza kufanga katika maeneo hayo na tunafahamu kwamba teknolojia ni dynamic, inabadilika mara kwa mara na sisi tumejipanga kuhakikisha tunahuisha mifumo hii ya udhibiti lakini pia ya kutambua changamoto za majanga ikiwepo moto kila mara.

Kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na nimpongeze kwa ufuatiliaji wake mzuri kwamba Serikali imeweka mfumo ambao utakuwa mara kwa mara unapitia na ku-update mifumo hiyo ili iweze kufanya kazi vizuri zaidi.

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu majengo ya zamani ni kweli kwamba mifumo hii sasa kwenye majengo mapya imekuwa sehemu ya michoro kuhakikisha kwamba inazingatia uwepo wa vifaa na miundombinu hiyo. Lakini tumetoa maelekezo katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa katika mikoa kote nchini kuhakikisha katika majengo yale ya zamani yakiwemo masoko, Ofisi za Serikali na maeneo kama hayo wanafunga mifugo ya kutambua na kudhibiti majanga ya moto, ahsante.