Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 137 2022-09-23

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka CCTV camera na alarm systems katika masoko, shule na sehemu za wazi zenye mkusanyiko?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lucy John Sabu, Mbunge wa Viti Maalumu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ili kudhibiti majanga mbalimbali katika taasisi, Serikali imekwishachukua hatua mbalimbali ambapo kupitia Mpango wa Uendelezaji Miji ya Kimkakati Tanzania na Mpango wa Uboreshaji wa Miji jumla ya miji 26 iliyotekeleza miradi ya kimkakati ya ujenzi wa masoko, stendi, na bustani za kupumzikia zimefungiwa vifaa vya utambuzi ikiwemo CCTV camera na alarm system. Aidha, ukarabati wa shule 89 kongwe na chakavu uliofanyika umezingatia miundombinu ya kujikinga na majanga hususani majanga ya moto.

Mheshimiwa Spika, Serikali imekwishatoa maelekezo katika Mikoa yote nchini kuzingatia ufungaji wa vifaa vya kutambua na kudhibiti majanga mbalimbali katika taasisi. Ahsante sana.