Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kubebea wagonjwa katika Kituo cha Afya Gidas?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza kwa kuwa magari yaliyonunuliwa ni 195 na halmashauri ziko 184 nchini; je, kati ya haya magari yaliyobaki moja litakwenda kwenye Kituo cha Afya cha Gidas?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa mahitaji ya wahudumu wa afya katika kituo hicho ni 32 na waliopo sasa ni nane tu; je, Serikali iko tayari kuongeza wahudumu wa afya ili kuboresha huduma za afya kwenye kituo hicho? Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Daniel Baran Sillo, Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba magari yatakayonunuliwa ni 195 lakini tuna halmashauri 184 na tutazama zile halmashauri au vituo ambavyo viko mbali zaidi maeneo ambayo ni hard to reach tutawapa kipaumbele kuwapa gari zaidi ya moja katika halmashauri hizo. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hoja ya Kituo cha Afya cha Gidas amesema kwa muda mrefu, tutakwenda kuona uwezekano wa kuwatafutia gari ili tuweze kuondoa changamoto ya wananchi katika eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, lakini pili, kuhusiana na watumishi ni kweli tunachangamoto ya upungufu wa watumishi, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo ameona Serikali imeendelea kuajiri watumishi na kuwapeleka kwenye vituo vya afya, tutahakikisha tunaendelea hivyo kwa awamu na tutatoa kipaumbele cha afya hicho cha Gidas. Ahsante.

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kubebea wagonjwa katika Kituo cha Afya Gidas?

Supplementary Question 2

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, na matatizo ya magari ya kubebea wagonjwa katika vituo vya afya; je, ni lini Serikali itapeleka magari hayo katika Kituo cha Afya cha Kisolya na kile cha Kasuguti?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Charles Kajege, Mbunge wa Jimbo la Mwibara kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, magari ya wagonjwa yatapeleka kwenye halmashauri zote 184 nchini kote na sasa ni maamuzi ya halmashauri kuona kipaumbele katika halmashauri yao ni kituo kipi cha afya ambacho kina uhitaji zaidi wa gari la wagonjwa.

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kubebea wagonjwa katika Kituo cha Afya Gidas?

Supplementary Question 3

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, katika Wilaya ya Arumeru kuna gari moja tu la kubebea wagonjwa; je, Serikali ina mkakati gani wa kupeleka gari la ziada katika Wilaya ya Arumeru?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zaytun Swai, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kati ya Oktoba na Novemba mwaka huu gari moja jipya la wagonjwa litapelekwa katika Halmashauri hii ya Arumeru. Ahsante.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kubebea wagonjwa katika Kituo cha Afya Gidas?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kuna halmashauri ambazo zina hospitali mbili za wilaya ikiwemo na halmashauri ninayotoka mimi ya Geita. Sasa Serikali itapeleka magari mawili kwa sababu ukipeleka gari moja linakuwa na mgongano wa hoja kwa sababu kuna hospitali mbili na Wabunge wawili tofauti.

Je, Serikali ipo tayari kupeleka magari mawili katika Halmashauri ya Geita?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, magari yanapelekwa kwenye halmashauri na halmashauri ziko 184 magari yako 195. Kwa hiyo, kila halmashauri ikiwepo halmashauri ya Mji wa Geita lakini pia Halmashauri ya Wilaya ya Geita watapata gari moja moja, ahsante.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kubebea wagonjwa katika Kituo cha Afya Gidas?

Supplementary Question 5

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kumekuwa na ahadi ya muda mrefu sana kupeleka gari ya wagonjwa katika Kituo cha Afya Mlola. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo kupeleka gari Kituo cha Afya Mlola?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shabani Shekilindi, Mbunge wa Jimbo la Lushoto kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, halmashauri ya Lushoto itapewa gari la wagonjwa jipya kati ya Oktoba na Novemba mwaka huu, kwa hivyo nimuombe Mheshimiwa Mbunge kwa kushirikiana na Mkurugenzi waone uwezekano wa kupeleka gari hili katika kituo cha afya cha kipaumbele kikubwa zaidi ikiwemo hicho ambacho amekitaja. Ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kubebea wagonjwa katika Kituo cha Afya Gidas?

Supplementary Question 6

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante, kutokana na umbali wa Kituo cha Afya Nanjilinji kutoka Makao Makuu ya Wilaya, lakini pia kutoka Hospitali ya Wilaya ya Kinyonga; je, Serikali itakubaliana nami kwamba upo umuhimu wa kupeleka gari la wagonjwa kwa umuhimu wake na upekee wake?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Kassinge, Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nikweli Kituo cha Afya Nanjilinji kiko mbali lakini kinahudumia wananchi wengi na Mheshimiwa Mbunge amekifuatilia na tumekubaliana kwamba katika vituo ambavyo vitapewa magari ni pamoja na Kituo cha Afya cha Nanjilinji.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kubebea wagonjwa katika Kituo cha Afya Gidas?

Supplementary Question 7

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Tarafa ya Simbayi na Tarafa ya Basuto katika Jimbo la Hanang tuna changamoto kubwa sana kwanza ya umbali na hakuna gari la wagonjwa; je, ni lini Serikali sasa itapeleka magari ya wagonjwa katika maeneo hayo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia Abdukarimu Halamga, Mbunge wa Viti Maalumu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tarafa hizi ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja alikwishazileta na pia kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge Hhayuma wamekuwa wakishirikiana kwa karibu sana na kuona wananchi wa Hanang wanapata huduma hizi na nimhakikishie tu kwamba Mheshimiwa Mbunge tumeshafanya tathinini ya kuona uwezekano wa kupeleka la wagonjwa lakini gari moja la wagonjwa jipya litaletwa Hanang ili muweze kupeleka katika tarafa hizo, ashante.