Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Khadija Shaaban Taya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA S. TAYA aliuliza: - Je, Serikali inatoa kauli gani kwa waajiri ambao wanasuasua katika kuwaajiri watu wenye ulemavu wenye sifa stahiki?

Supplementary Question 1

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri.

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita, imeanzisha vyuo vya watu wenye ulemavu, kati ya mafunzo ambayo wanayotoa pale mojawapo ni kutengeneza viatu na hapo hapo katika Wizara hii hii wamefungua kiwanda cha kutengeneza viatu pale magereza Mkoa wa Kilimanjaro; je, katika hiki kiwanda walemavu wameajiriwa na kama wameajiriwa ni wangapi?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, kwa kuthibitisha spirit ile ile ya Serikali ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan katika utekelezaji mzuri wa sheria hii ya watu wenye ulemavu, katika kile kiwanda ambacho Mheshimiwa Mbunge amekitaja zoezi bado kwanza kiko katika hatua ya awali ya kuanza kufanya mobilization na ukamilishaji wa ujenzi bado haujatimia.

Mheshimiwa Spika, lakini katika uthibitisho wa hilo kwamba tunazingatia hili kama Serikali, Ofisi ya Rais – TAMISEMI kwa kuratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu katika nafasi za walimu 8,000 zilizotoka mwaka 2020 watu wenye ulemavu 242 waliajiriwa ambao ni asilimia 3.2. Sambamba na hiyo katika nafasi za mwaka 2021 za ualimu zilizotolewa zilikuwa nafasi 6,949 watu wenye ulemavu 145 waliajiriwa ambao ni sawa na asilimia mbili.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo pia mwaka 2022 katika usimamizi na utekelezaji mzuri wa Serikali ya Awamu ya Sita, ajira zilizotolewa 9,800 za nafasi ya ualimu watu wenye ulemavu 261 walipata sawa na asilimia
2.66. Katika sekta ya afya na maeneo mengi sababu ya muda nafasi 7,612 ambazo zilitolewa watu wenye ulemavu waliopata nafasi hiyo ni 0.63 kulingana na sifa na vigezo ambavyo viliwekwa.

Mheshimiwa Spika, katika Serikali hii tumeweka minimum standard, kwamba hata vile viwango vya ufaulu tunaviangalia katika hali ambayo yule anakuwa sifa kwa sababu watu wenye ulemavu wanakuwa wachache katika uombaji wa nafasi hii.

Kwa hiyo, tutaendelea kuzingatia sheria na kuhakikisha kwenye private sector na Serikali tunazingatia takwa hili la kisheria la kuajiri watu wenye ulemavu, kwa sababu kufanya hivyo pia ni ibada kwa nchi.