Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 135 2022-09-23

Name

Khadija Shaaban Taya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA S. TAYA aliuliza: -

Je, Serikali inatoa kauli gani kwa waajiri ambao wanasuasua katika kuwaajiri watu wenye ulemavu wenye sifa stahiki?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa niaba ya Wazir Mkuu naomba kujibu swali namba 135 lililoulizwa na Mheshimiwa Khadija Shaaban Taya, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mnamo mwaka 2010, Serikali ilitunga Sheria ya Watu wenye Ulemavu Na. 9 kwa lengo la kusimamia masuala mbalimbali ya watu wenye ulemavu. Katika kifungu cha 31(1) kinaeleza kuwa kila mwajiri wa umma au binafsi, endapo kutatokea nafasi ya ajira na mtu mwenye ulemavu aliyekidhi viwango vya chini vya ajira hiyo akaomba atalazimika kumwajiri. Aidha, kifungu 31(2) cha Sheria ya Watu wenye Ulemavu Na. 9 ya 2010 kinaeleza kuwa kila mwajiri mwenye waajiriwa kuanzia 20 na kuendelea anatakiwa kuwa na watu wenye Ulemavu wasiopungua asilimia tatu ya waajiriwa wake.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia takwa hili la sheria naomba kuwakumbusha waajiri wote kuzingatia viwango hivyo vya ajira kama vilivyoelekezwa katika sheria na tutaendelea kufanya kaguzi na kuchukua hatua kwa wasiotekeleza takwa hilo la msingi la kisheria na kibinadamu.