Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asya Mwadini Mohammed

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASYA MWADINI MOHAMMED aliuliza: - Je, kuna viwanda vingapi vya kuchakata taka ngumu nchini?

Supplementary Question 1

MHE. ASYA MWADINI MOHAMMED: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Kwa mujibu wa majibu ya Mheshimiwa Waziri ni dhahiri kwamba Tanzania hakuna kiwanda kinachochakata vigae na ukizingatia vigae vingi tunaingiza kwanza chupa za pombe na mengineyo, lakini tunazalisha na hapa nchini maana yake uchafuzi wa kimazingira unaendelea. Nini mkakati wa Serikali kuanzisha kiwanda cha kuchakata vigae nchini?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; je, Serikali haioni sasa kupunguza kodi kwa bidhaa zote zinazochakatwa na taka ngumu ili kuweza kuwavutia wawekezaji waweze kuwekeza nchini lakini pia na kuyalinda mazingira yetu?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Asya Mwadini Mohamed Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli bado hatuna viwanda vya kuchakata vigae kwa maana ya mabaki, lakini nia ya Serikali ni kuendelea kuweka mazingira wezeshi ya kuvutia wawekezaji ambao tunaamini wataendelea kuwekeza katika maeneo tofauti ikiwemo hili ambalo Mheshimiwa Mbunge amelitaja, kwa hiyo tunaendelea kutafuta na kuweka kuwavutia wawekezaji katika eneo hili.

Mheshimiwa Spika, lakini la pili ni kweli Serikali tunaendelea kufanya juhudi na kuona namna ya kuweka vivutio maalum katika maeneo mbalimbali ikiwemo hili la kupunguza kodi katika maeneo ya uchakataji au urejeshaji taka ambazo kwa kweli zinaharibu sana mazingira hapa nchini. Kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira tunaendelea na juhudi za kuhakikisha tunatunza mazingira kwa kuvutia wawekezaji wanaopunguza taka ambazo zimezagaa mjini nakushukuru.