Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 18 2022-09-13

Name

Asya Mwadini Mohammed

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASYA MWADINI MOHAMMED aliuliza: -

Je, kuna viwanda vingapi vya kuchakata taka ngumu nchini?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asya Mwadini Mohammed, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Tanzania hadi sasa tuna jumla ya viwanda 137 vya kuchakata taka ngumu hapa nchini. Viwanda hivyo vimegawanyika katika makundi manne ambayo ni viwanda vinavyotumia taka zitokanazo na chuma viko 16; viwanda vinavyotumia taka za plastiki viko 70; viwanda vidogo vya kutengeneza mkaa mbadala kutoka kwenye mabaki ya kilimo viko 50; na tuna kiwanda kimoja cha kutengeneza mbolea aina ya mboji inayotokana na mabaki ya vyakula. Nakushukuru.