Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Chuo cha VETA unaoendelea Wilayani Mkinga utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hivi tunavyozungumza chuo hiki hakina mkufunzi hata mmoja wala hakina Mkuu wa Chuo. Wakufunzi wanaotegemewa ni kutoka Chuo cha VETA Tanga ambacho na chenyewe kimeelemewa, kinategemewa chuo hichohicho cha Tanga kitoe wakufunzi kwenda Korogwe. Je, Serikali ina mpango gani wa haraka kuhakikisha kinapata wakufunzi ili hayo malengo ya kuanza mwezi wa Kumi yaweze kutimia? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Hivi tunavyozungumza vifaa vya ufundi havijapatikana kwenye vyuo hivi vya Mkinga wala Korogwe. Serikali ina mkakati gani wa haraka kuhakikisha vifaa hivi vinapatikana ili mafunzo yaweze kufanyika? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba sasa kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kitandula Mbunge wa Mkinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nikiri ni kweli tuna upungufu wa walimu kwenye vyuo vyetu hivi vya VETA hivi sasa tuna Wilaya 77 zenye Vyuo vya VETA vya Wilaya pamoja na mikoa. Lakini nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 Wizara imepata kibali cha kuajiri walimu zaidi ya 514. Kwa hiyo, tayari mchakato huu wa kuajiri walimu uko kwenye hatua za mwisho na tutahakikisha sasa miongoni mwa walimu hawa 514 tunaokwenda kuwaajiri basi waweze kwenda kwenye Chuo cha Mkinga lakini pamoja na vile vyuo 25 vya Wilaya pamoja na vyuo vile vinne vya mikoa ambavyo sasa nakamilisha ujenzi wake.

Mheshimiwa Spika, katika eneo la pili amezungumzia suala la vifaa vya kufundishia; ni kweli mchakato wa vifaa unaendelea kwa sababu upo kwenye bajeti 2022/2023 ambao tumeanza kuutekeleza hivi sasa na tuko katika quarter ya kwanza. Kwa hiyo, pindi fedha zitakapokuwa zimekaa tayari tunakwenda kununua hivyo vifaa na kuvipeleka kwenye vyuo hivi ambavyo tayari vimekamilika, lakini upande wa samani zote za vyuo vyote 25 viko tayari kwa ajili ya kupelekwa katika maeneo haya nakushukuru sana.