Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amina Daud Hassan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA DAUDI HASSAN aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutoa elimu kwa Wanawake kuepuka ndoa za siri ambazo zina changamoto ya malezi ya familia?

Supplementary Question 1

MHE. AMINA DAUDI HASSAN: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali italeta marekebisho ya Sheria ya Ndoa ili iweze kupunguza changamoto ya ndoa za siri na za utotoni?(Makofi)

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Amkina Daudi Hassan, kuhusu Sheria ya Ndoa na Marekebisho yake.

Mheshimiwa Spika, wiki ijayo Kamati ya Maendeleo ya Jamii pamoja na Kamati ya Sheria na Katiba zinaketi kikao kwa ajili ya kufanya marekebisho ya Sheria ya Ndoa. Hivyo, basi tumepokea hoja yake, tunaenda kuwasilisha tujumuishe ili vijadiliwe pamoja. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA DAUDI HASSAN aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutoa elimu kwa Wanawake kuepuka ndoa za siri ambazo zina changamoto ya malezi ya familia?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na sheria za ndoa, lakini kuna tatizo kubwa sana la malezi kwa watoto wetu. Kuna changamoto kubwa sasa hivi ya wazazi kuwapeleka watoto wadogo kuanzia nursery school mpaka sekondari katika shule za boarding na watoto kukosa malezi ya wazazi. Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha sasa mitaala inarudishwa kwa mfano ile ya sayansikimu katika shule zetu ili watoto waweze kupata malezi na kupata elimu za kujitegemea?

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la Mheshimkiwa Dkt. Ritta Kabati la nyongezab kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumepokea hoja yako. Ni kweli, kuna kasi kubwa ya mmomonyoko wa maadili inayoendelea na inasababisha masuala mengi sana ya visa vya ukatili. Kwa sababu marekebisho ya mitaala yanaangukia sekta nyingine tumelipokea tutakwenda kukaa tulijadili kwa pamoja, tujange hoja tuone namna gani tunaweza tukafanya ili kurekebisha hiyo mitaala ikidhi na kuakisi changamoto za sasa kwa ustawi wa Taifa letu la kesho.