Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Community Development, Gender and Children Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum 15 2022-09-13

Name

Amina Daud Hassan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA DAUDI HASSAN aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kutoa elimu kwa Wanawake kuepuka ndoa za siri ambazo zina changamoto ya malezi ya familia?

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Amina Daudi Hassan, Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa ndoa ni Taasisi muhimu katika kuimarisha haki na ustawi wa familia. Hivyo, Serikali kupitia utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto wa mwaka 2017/2018 hadi 2021/2022 eneo namba nne linalohusu malezi na mahusiano ya familia imeendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu malezi chanya na mahusiano ndani ya familia ili kuwa na familia inayozingatia maadili mema.

Mheshimiwa Spika, Serikali pia ipo kwenye hatua za mwisho za kukamilisha Mwongozo wa Taifa wa Uendeshaji, Usimamizi na Uratibu wa Mabaraza ya Usuluhishi wa Ndoa na Familia ambao utasaidia kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa kuzingatia taratibu za ufungaji wa ndoa pamoja na kuyajengea mabaraza ya usuluhishi wa migogoro ya ndoa na familia uwezo ili kuendelea kutoa elimu katika jamii.