Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Suleiman Haroub Suleiman

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. SULEIMAN HAROUB SULEIMAN aliuliza: - Je, ni vigezo gani vinatumika kuchagua wachezaji wa timu ya Taifa (Taifa Stars)?

Supplementary Question 1

MHE. SULEIMAN HAROUB SULEIMAN: Mheshimiwa Spika, ahsante sana pamoja na majawabu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina swali moja lenye kifungu (a) na (b) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, timu ya Taifa Stars ni timu ya Tanzania na Tanzania ina ligi kuu mbili kwa maana ya kwamba Ligi Kuu ya Zanzibar na Ligi Kuu ya Tanzania Bara. Sasa je, kwenye kuchagua wachezaji kwenye kutafuta wachezaji kuunda timu ya Taifa hauoni haja au hauoni sababu kwamba sasa kocha wa timu ya Taifa kuweza kudhuru ligi zote mbili ili kupata wachezaji wazuri?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; zamani kulikuwa kuna ligi kuu ya Muungano kwa maana ya Super Cup ligi ile iliweza kutoa timu bora na timu nyingi ambazo zilishiriki ligi ile ilitoa wachezaji wa timu ya Taifa Stars. Sasa je, Serikali ina mkakati gani kuweza kurudisha kombe hili? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kunipa nafasi nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Suleiman kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Suleiman amependa kufahamu kwamba katika kuandaa timu za Taifa; je, si vyema timu hizi zikaandaliwa kwa kufatilia ligi zote mbili za TFF pamoja na ZFF.

Mheshimiwa Spika, hili ni dhahiri kwamba tunapochagua wachezaji wa timu ya Taifa kocha hakatazwi kwenda popote kwenye hizi ligi ndani ya Taifa letu na hili limekuwa likifanyika ndio maana wachezaji katika timu yetu ya Taifa wanatoka pia kwa upande wa Zanzibar pamoja na upande wa Bara. (Makofi)

Kwa hiyo hili tutaendelea kuimarisha tukishirikiana na ZFF pamoja na TFF ili kuhakikisha kwamba tunapata wachezaji wazuri na hata katika benchi la ufundi tumekuwa tukiwahusisha wenzetu wa Zanzibar kuhakikisha pia wanatoa mchango na wanakuwa sehemu ya ligi yetu na timu yetu ya Taifa.

Mheshimiwa Spika, swali la pili amependa kufahamu tulikuwa na ligi ya Muungano sasa anapenda kufahamu ni ligi hii itarudishwa? Nijibu hili kwamba jambo hili sisi kama Wizara pia tumeliona. Tumekuwa sasa na mazungumzo kati ya BMT, TFF pamoja na ZFF kuhakikisha kwamba ligi hii inarudishwa.

Mheshimiwa Spika, mwanzoni ilisitishwa kwa sababu Zanzibar ilipata associate membership kwa CAF wakawa wanapeleka timu zao mbili na huku Bara pia wakawa wanapeleka pia timu zao mbili. Lakini kwa afya ya Muungano wetu, kwa afya ya mashirikiano tuliyonayo kama Taifa tumekubaliana na kamati imeshaundwa ligi hii itarudishwa hivi karibuni tunaangalia tu tathmini na gharama kwamba gharama zitakuwaje, lakini itarudishwa. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. SULEIMAN HAROUB SULEIMAN aliuliza: - Je, ni vigezo gani vinatumika kuchagua wachezaji wa timu ya Taifa (Taifa Stars)?

Supplementary Question 2

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Mheshimiwa Waziri anasema moja ya kigezo cha wachezaji kuteuliwa katika timu ya Taifa ni kupata muda wa kutosha kwa maana ya play time katika ligi za juu kwa maana ya premier na first division. Wachezaji wa Tanzania wanapata vipi nafasi kiasi hicho wakati ligi zetu zimejaa wageni walio wengi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kunipa nafasi, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tarimba Abbas kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni dhahiri kwamba hili ni la msingi, lakini sisi tuna limitation ya usajili wa wachezaji wa nje katika timu. Hata wanapocheza wanapoingia uwanjani kocha anazingatia pia kuna uwakilishi wa vijana wetu katika mechi hiyo ya siku hiyo. Tutaendelea kulizingatia na tutaendelee kushauri TFF wahakikishe pamoja na kwamba wamesajili wachezaji kutoka nje kwa limit ile ambayo tumewapa kupitia BMT vijana wetu wanapata nafasi wacheze waoneshe vipaji vyao, ahsante.