Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 12 2022-09-13

Name

Suleiman Haroub Suleiman

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. SULEIMAN HAROUB SULEIMAN aliuliza: -

Je, ni vigezo gani vinatumika kuchagua wachezaji wa timu ya Taifa (Taifa Stars)?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nikushukuru na kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Suleiman Haroub Suleiman, Mbunge wa Baraza la Wawakilishi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, jukumu la kusimamia timu zote za Taifa ni la Serikali kwa kushirikiana na Vyama na Mashirikisho ya Michezo. Kwa mujibu wa Kamati ya Ufundi ya TFF vigezo vinavyotumika kuchagua wachezaji wa Taifa Stars ni kama ifuatavyo; mchezaji awe raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mchezaji anayecheza katika klabu ya ligi za juu, mchezaji anayepata nafasi na kucheza kwenye klabu husika (playing time), mchezaji awe na ufanisi mzuri wa kucheza (good performance), awe na vigezo katika nafasi anayocheza (fitting the positional profile), pamoja na kuwa na nidhamu ya kiuchezaji na nidhamu katika maisha ya kawaida.