Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:- Kumekuwa na wimbi kubwa la wanafunzi wa shule za Serikali za msingi na sekondari wanaofeli kutokana na kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi katika darasa moja dhidi ya mwalimu mmoja kwa wanafunzi huku wakifundishwa kuanzia saa moja na nusu hadi saa kumi na nusu jioni, na kufanya walimu wakose muda wa kutosha wa kusimamia kazi za wanafunzi. Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na changamoto hizo?

Supplementary Question 1

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali ya nyongeza na nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa sababu kuu za ufaulu duni ni miundombinu mibovu ya ufundishaji na kujifunza. Je, Serikali imeweka mkakati gani kwa shule za Njombe?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa waathirika wakuu ni wasichana, kwa sababu wanapewa kazi nyingi na wazazi wao majumbani, je, Serikali ina mkakati gani kumsaidia mtoto huyu wa kike?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la miundombinu mibovu, hili ni kama tulivyosema katika bajeti yetu ya mwaka huu wa fedha kwamba tumeelekeza katika maeneo mbalimbali ili angalau kuongeza speed kwenye hii changamoto tuliyo nayo hivi sasa ya wanafunzi wengi sana tuliowasajili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo vilevile kuwafanya walimu wafundishe katika mazingira rafiki. Ndiyo maana katika bajeti ya mwaka huu mkoa wa Njombe peke yake tumetenga kiwango cha fedha cha kutosha ili kuhakikisha maeneo mbalimbali yanaweza kufikiwa. Ndiyo maana tukifanya rejea ya bajeti yetu tuliyopitisha hapa hapa, siwezi kukupa takwimu halisi, lakini tumeugusa Mkoa wa Njombe kuangalia kipaumbele hicho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala zima la miundombinu Mheshimiwa Mbunge nadhani na wewe ni mpiganaji mzuri katika eneo hilo. Ukiachia miundombinu, vilevile miongoni mwa mambo ambayo yanachangia sana ni suala zima la malezi. Wakati mwingine wazazi wanakuwa irresponsible, hawawajibiki vya kutosha kuhakikisha watoto wao wanawasimamia kwa karibu.
Mheshimiwa Mbunge nikuhakikishie wakati napita pita maeneo mbalimbali, kuna maeneo mengine utakuta madarasa yapo ya kutosha, hali kadhalika walimu wa kutosha lakini shule zile tulizozipitia hakuna hata mwanafunzi aliyepata division one au division two. Kwa bahati mbaya zaidi unaweza kukuta walimu wengi wa sayansi hakuna lakini wa arts wapo na bado huwezi ukaona “C” moja au “B” moja ya Kiswahili wala ya civics; ni kwamba concentration ya watoto imekuwa chini. Kwa hiyo, jukumu letu kubwa sambamba na kuongeza miundombinu tuna changamoto kubwa ya kuwahamasisha wazazi kusimamia suala zima la taaluma za watoto wao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuwaokoa vijana wetu wa kike. Ni kweli suala la mimba kwa watoto wa kike limekuwa kubwa, ndiyo maana mchakato wetu sasa hivi ni tunajielekeza katika ujenzi wa shule za sekondari za bweni hasa kwa upande wa wanawake. Lengo letu ni kuhakikisha zile changamoto zinawapata watoto wanapokwenda shuleni ziweze kupungua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wa Afya wiki iliyopita alisema kwamba wale mabaradhuli wanaohakikisha wanaharibu watoto wa watu, tuhakikishe wanachukuliwa hatua kali ili hawa watoto wa kike waweze kupata elimu yao kama ilivyokusudiwa.

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:- Kumekuwa na wimbi kubwa la wanafunzi wa shule za Serikali za msingi na sekondari wanaofeli kutokana na kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi katika darasa moja dhidi ya mwalimu mmoja kwa wanafunzi huku wakifundishwa kuanzia saa moja na nusu hadi saa kumi na nusu jioni, na kufanya walimu wakose muda wa kutosha wa kusimamia kazi za wanafunzi. Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na changamoto hizo?

Supplementary Question 2

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kumekuwa na tabia ya walimu kuto-report kwenye mikoa ambayo inaitwa mikoa ya pembezoni kama Mkoa wetu wa Lindi. Je, kuna mkakati gani mwaka huu wa kuhakikisha kwamba walimu watakaopangwa watakwenda Lindi kutatua tatizo kubwa la walimu lililopo kwenye shule zetu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, wiki iliyopita nilisema kwamba kuna tatizo, si mkoa wa Lindi peke yake, ukienda Katavi, Kigoma, Mara, Sumbawanga na maeneo mengine. Tumesema mwaka huu tu tunaajiri walimu wapatao 35,000, lakini walimu wengine wakipelekwa kule hawaendi; na kwa bahati mbaya wengine wakienda wanataka kuishia pale pale mjini. Na ndiyo maana tumetoa maelekezo mwaka huu kwamba walimu wote watakaokwenda ku-report wahakikishe wanafika vituoni.
Naomba kutoa rai, mwaka huu tumepeta maombi mengi sana ya walimu ambao ndani ya miaka mitatu, minne walishindwa ku-report wakaenda private schools, sasa hivi private schools hali imekuwa mbaya, wanakuja kuomba tena ajira Serikalini.
Tuombe kutoa maelekezo; kwamba walimu watakaoshindwa kufika katika vituo vyao wasitarajie kuja kuomba mwakani baada ya kuona kwamba wamekosa nafasi katika private schools. Hili ni agizo letu na tutaenda kulisimamia kwa nguvu zote.