Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 20 Education, Science,Technology and Vocational Training, Ofisi ya Rais TAMISEMI. 166 2016-05-16

Name

Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:-
Kumekuwa na wimbi kubwa la wanafunzi wa shule za Serikali za msingi na sekondari wanaofeli kutokana na kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi katika darasa moja dhidi ya mwalimu mmoja kwa wanafunzi huku wakifundishwa kuanzia saa moja na nusu hadi saa kumi na nusu jioni, na kufanya walimu wakose muda wa kutosha wa kusimamia kazi za wanafunzi.
Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na changamoto hizo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lucia Michael Mlowe, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuboresha elimu nchini kwa kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani, Serikali imeendelea kutenga bajeti kila mwaka kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule za msingi na sekondari. Katika mwaka wa fedha 2015/2016, Serikali ilitenga shilingi bilioni 67.83 ambazo zimepokelewa na zimetumika ka ajili ya ukarabati, ujenzi na umaliziaji wa vyumba vya madarasa, vyoo vya walimu na wanafunzi, ujenzi wa nyumba sita (multiple unit houses) na uwekaji wa umeme (grid house solar) katika shule za sekondari 528 nchini kote. Katika bajeti ya mwaka 2016/2017 zimetengwa shilingi bilioni 48.3 kwa ajili ya kazi hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na juhudi katika ujenzi wa miundombinu, Serikali inatarajia kuajiri walimu wapya 35,411 kwa shule za msingi na sekondari ili kuongeza idadi ya walimu hivyo kupunguza mzigo mkubwa uliopo kwa walimu kwa lengo la kuongeza tija katika sekta ya elimu hapa nchini.