Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ramadhan Suleiman Ramadhan

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN K.n.y. MHE. TOUFIQ SALIM TURKY aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani juu ya mfumuko wa bei unaoendelea nchini?

Supplementary Question 1

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ingawa, Mheshimiwa Naibu Waziri amejibu vizuri kwenye swali la msingi, lakini naomba niulize swali la nyongeza. Serikali imeshafanya jitihada za makusudi kwenye kupunguza ukali kwenye bidhaa ya mafuta. Je, Serikali haioni haja ya kufanya jitihada hizo hizo ili kupunguza ukali kwenye bidhaa za vyakula?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ramadhan, Mbunge wa Chake Chake, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi kwamba tayari Serikali imeshatoa ruzuku kwa upande wa mbolea na tayari Serikali imeshusha kodi ya uingizaji wa mafuta ya kula. Kwa hiyo, Serikali imeshachukua hatua ya kupunguza ukali wa mfumuko wa bei za mafuta.

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN K.n.y. MHE. TOUFIQ SALIM TURKY aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani juu ya mfumuko wa bei unaoendelea nchini?

Supplementary Question 2

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nimpongeze Waziri kwa majibu yake mazuri, lakini naomba niulize swali la nyongeza. Serikali imekuwa na majibu mazuri sana kuhusu mfumuko wa bei, lakini uhalisia ulivyo nje katika mitaa na vijiji, hali ilivyo haiko hivyo ambavyo Serikali imekuwa ikijibu. Je, Serikali inaliambia nini Taifa letu la Tanzania juu ya mfumko huu wa bei?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ussi Pondeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali na mipango yake ya Serikali ni kusimamia bei za bidhaa na kuona kwamba wananchi wanapata huduma zao kwa bei nafuu. Ahsante.