Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 6 2022-09-13

Name

Toufiq Salim Turky

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpendae

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN K.n.y. MHE. TOUFIQ SALIM TURKY aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani juu ya mfumuko wa bei unaoendelea nchini?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Toufiq Salim Turky, Mbunge wa Mpendae, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mwaka 2021/2022, mfumuko wa bei uliongezeka na kufikia wastani wa asilimia 4.0 ikilinganishwa na asilimia 3.3 katika kipindi kama hicho mwaka 2020/2021. Pamoja na ongezeko hili, mfumuko wa bei umeendelea kubaki kwenye wigo wa tarakimu moja na upo ndani ya lengo la Jumuiya ya Afrika Mashariki la asilimia 8.0 na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika la kati ya asilimia 3.0 hadi 7.0.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na mikakati mbalimbali ikiwemo: kuimarisha sekta za uzalisha ili kuongeza upatikanaji wa bidhaa unaoendana na mahitaji; kutoa ruzuku kwa ajili ya kupunguza bei ya nishati ya mafuta kiasi cha shilingi bilioni 100 kwa mwezi ambapo shilingi bilioni 500 zimetengwa; kutoa ruzuku ya pembejeo za mbegu na mbolea na kutoa unafuu wa kodi katika uagizaji wa baadhi ya bidhaa muhimu.

Mheshimiwa Spika, Serikali inachukua hatua nyingine katika suala hili ikiwemo: kuruhusu watu wenye uwezo wa kuleta mafuta kwa bei nafuu; kuanzisha mfuko wa kuhimili ukali wa bei za mafuta baada ya bei za mafuta kutulia katika soko la dunia; kuanzisha hifadhi ya mafuta ya kimkakati na kuanzisha upokeaji wa mafuta katika ghala moja. Ahsante.