Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuunda Kikosi Kazi kuratibu Mikataba ya mazingira na mabadiliko ya Tabianchi kati ya Tanzania Bara na Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Napenda kumpongeza Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa mashirikiano haya hayapo kisheria: Je, Serikali haioni haja ya kuwa na utaratibu wa kisheria ili kuwezesha ushiriki wa Zanzibar kuwa bora zaidi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili: Je, mpaka kufikia Julai, 2022, Zanzibar imenufaika na miradi gani ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Kusini Pemba, Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ushirikiano na majadiliano ambayo huwa tunafanya yanayohusiana na mikataba ya Kimataifa, ya mazingira na kukabiliana na mazingira ya tabia ya nchi, ni ya kisheria. Maana yake, yako kisheria. Hata ukienda ukisoma Katiba ya Jamhuri kwenye fungu lile la Foreign Affairs utakuta kumeelezwa namna ambavyo inatakiwa tushirikiane kwenye mahusiano yanayohusu masuala ya mikataba ya Kimataifa.

Mheshimiwa Spika, hata ukienda kwenye sheria yetu ya mazingira, imeeleza, Waziri anayehusika na mazingira kwa upande wa Jamhuri ya Muungano, basi anatakiwa akae na ashirikiane na Waziri anayehusika na mazingira kwa upande wa Zanzibar. Kwa hiyo, majadiliano haya hasa mikataba ya Kimataifa yanakuwa yapo kisheria zaidi.

Mheshimiwa Spika, ipo miradi ambayo imetekelezwa na inaonekana. Kwa mfano, kuna ujenzi wa kuta ama kingo za kuzuia maji Wete kule Sepwese, hiyo ipo; pia kuna miradi ya kurejesha ardhi iliyoathirika na mabadiliko ya tabia ya nchi, hii iko maeneo ya Kiuyu, Shumba Viamboni, Shumba Mjini, Maziwa Ng’ombe maeneo mingine miradi hii ipo na imepita.

Mheshimiwa Spika, pia upo mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi maeneo ya Kaskazini A, Unguja katika Mkoa wa Kaskazini.

Mheshimiwa Spika, nashukuru.