Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 4 2022-09-13

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kuunda Kikosi Kazi kuratibu Mikataba ya mazingira na mabadiliko ya Tabianchi kati ya Tanzania Bara na Zanzibar?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Maryam Azan Mwinyi, Mbunge wa Viti Maalum, kutoka Mkoa wa Kusini Pemba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi mwanachama wa mikataba mbalimbali ya Kimataifa ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira ambayo inaratibiwa chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano.

Mheshimiwa Spika, kwa msingi huo, utaratibu unaotumika katika kuratibu masuala ya mikataba ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi kwa pande zote mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni wa kushirikiana katika majadiliano ya pamoja na kushiriki katika mikutano ya Kimataifa na utekelezaji wa Mikataba hiyo.

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikishirikiana kwa karibu na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika kutekeleza program na miradi mbalimbali ya hifadhi na usimamizi wa mazingira inayotekelezwa chini ya mikataba husika.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)