Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaigawa Kata ya Katumba?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri, lakini kwa kuwa mtendaji ni mmoja na watendaji wa vijiji wako wawili tu, kata ni kubwa, ina vijiji 16: Ni lini Serikali itaongeza watendaji kwa ajili ya kata hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kutokana na mazingira magumu ya kata hiyo, vijiji 16 na mazingira magumu: Ni lini Mtendaji wa Kata ya Katumba anaweza kupata usafiri kwa ajili ya kufanya kazi kwa ufanisi zaidi? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Nsimbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatambua kwamba kata hii ni kubwa, ina vijiji 16 na inahitaji nguvu zaidi kwa watendaji wa kata kuhakikisha kwamba wanatoa huduma na pia watendaji wa vijiji. Naomba nilichukue jambo hili, tutalifanyia kazi na nitawasiliana naye kuhakikisha kwamba kata hii inaongezewa nguvu ya watendaji. Ahsante.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaigawa Kata ya Katumba?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa mahitaji makubwa ya wananchi ni kupata vitongoji vipya na vijiji vipya; na kwa kuwa mchakato huu haueleweki sana kwao, sisi tunalalamikiwa: Je, Serikali ina utaratibu gani sasa wa kugawa vijiji na vitongoji na mitaa ili kurahisisha huduma kwa wananchi? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zacharia Issaay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna mahitaji ya kugawa vijiji, vitongoji, kata na mara nyingine hata Halmashauri katika nchi yetu, lakini kama nilivyotangulia kujibu kwenye maswali ya msingi kwamba kipaumbele chetu sasa Serikali ni kuboresha kwanza miundombinu katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, utaratibu ni kwamba wananchi wanafanya vikao vyao vya Halmashauri za Kijiji na kwenda DCC na RCC na baadaye kuwasilisha maombi Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Kwa hiyo, namwombe Mheshimiwa Mbunge waanze taratibu hizo za kisheria wakati tukisubiri maamuzi ya Serikali kuja kugawa maeneo mengine ya kiutawala. Ahsante.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaigawa Kata ya Katumba?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kata ya Rungwe Mpya iliyoko Jimbo la Kasulu Vijijini ina idadi kubwa ya watu wengi sana: Je, ni lini Serikali itakubali kuigawa kata hiyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu la nyongeza la Mheshimiwa Josephine Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itagawa kata hizo baada ya kuwa tayari imeshaboresha miundombinu kwenye maeneo ya utawala yaliyopo sasa. Tuna kata nyingi na vijiji ambavyo bado vinahitaji uboreshaji. Kwa hiyo, baada ya hapo tutakwenda pia kutazama Kata hii ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja. Ahsante.

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaigawa Kata ya Katumba?

Supplementary Question 4

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Mlowo ni moja kati ya kata kubwa sana katika Mkoa wetu wa Songwe: Ni hatua zipi Serikali imefikia katika mchakato wa kuigawa kata hii?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Kata ya Mlowo ni moja ya kata kubwa, lakini utaratibu ni kwamba, endeleeni na taratibu za kuwasilisha maombi kwa mujibu wa taratibu za ugawaji wa maeneo ya utawala. Hata hivyo kipaumbele kwa sasa ni kuhakikisha tunaboresha miundombinu kwenye kata zilizopo kabla hatujakwenda kugawa kata hizi nyingine. Ahsante.