Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 3 2022-09-13

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaigawa Kata ya Katumba?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe Mbunge wa Jimbo la Nsimbo kama ifuatavyo: -

Mheshimwa Spika, Serikali inatambua uhitaji wa kuigawa Kata ya Katumba kutokana na ukubwa wake na idadi kubwa ya watu.

Mheshimiwa Spika, kutokana na kuwepo kwa maeneo mengi ya utawala ambayo bado hayana miundombinu muhimu ya kiutawala na ya huduma za jamii, Serikali kwa sasa imeweka kipaumbele zaidi katika kujenga miundombinu hiyo ili kutoa huduma bora kwa wananchi badala ya kuanzisha maeneo mapya ya utawala.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo inashauriwa kukamilisha hatua za maombi na kuwa na subira katika kipindi hiki mpaka hapo Serikali itakapoona inaweza kuigawa Kata hiyo. Ahsante sana.