Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je ni lini Serikali itafanya ukarabati wa nyumba za makazi ya askari wa Jeshi la Polisi kwenye Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Igunga?

Supplementary Question 1

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, nyumba hizi tunazoziongelea kama alivyosema Naibu Waziri zipo nne na zinakaa familia 20 zilijengwa mwaka 1993 nakumbuka mimi nilikuwa darasa la kwanza; sasa zimechakaa sana na zinahatarisha usalama wa askari wetu. Mimi ninachoomba ni commitment ya Serikali na mwaka jana kwenye bajeti niliongelea. (Makofi)

Ni lini watatuweka katika kipaumbele cha kuzijenga nyumba hizi ili tusihatarishe maisha ya askari wetu? Hilo la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili Naibu Waziri je, atakuwa tayari baada ya hili Bunge kuahirishwa apite Igunga, tuweze kwenda kuona hali halisi ambayo naiongelea hapa kabla maafa hayajatokea kuathirisha maisha? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawii ya nyongeza ya Mheshimiwa Ngassa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu commitment tunayo kama nilivyokwisha eleza tumefanya tathmini gharama zinajulikana, tutaanza awamu kwa awamu kukarabati nyumba ambazo zina hali mbaya sana. Kwa maana hiyo tutakapokuwa tunamaliza shughuli za Bunge katika ziara yangu niliyokwisha ahidi kutembelea Sumve - Mwanza, tutapita Igunga kuona kiwango cha uchakavu ili kuipa kipaumbele katika ukarabati wa nyumba hizo. Nashukuru. (Makofi)

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je ni lini Serikali itafanya ukarabati wa nyumba za makazi ya askari wa Jeshi la Polisi kwenye Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Igunga?

Supplementary Question 2

MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itamalizia na kukarabati ujenzi wa nyumba za polisi katika kituo cha polisi Wilaya ya Micheweni? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwisha jibu katika swali langu la msingi, Micheweni ambako kunahitajika pia ujenzi wa nyumba na kuboresha kituo ni miongoni mwa vituo ambavyo vitaimarishwa kulingana na mpango wetu wa kukarabati nyumba na vituo chakavu. Nashukuru. (Makofi)

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je ni lini Serikali itafanya ukarabati wa nyumba za makazi ya askari wa Jeshi la Polisi kwenye Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Igunga?

Supplementary Question 3

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati makazi ya askari polisi Wilaya ya Mbagala ambayo yana hali mbaya sana, sana, sana pamoja na kituo cha polisi cha Wilaya ya Mbagala? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Kisangi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, niliahidi tarehe 22 Februari nitakuwa Dar es Salaam naomba Mbunge awe tayari tuzunguke naye kwenye maeneo ya Mbagala, kuona kiwango cha uchakavu ili kwa pamoja tutafakari namna ya kuboresha majengo hayo kupitia bajeti yetu tunayotoa kila mwaka. Ahsante. (Makofi)