Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 14 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 167 2022-02-18

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: -

Je ni lini Serikali itafanya ukarabati wa nyumba za makazi ya askari wa Jeshi la Polisi kwenye Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Igunga?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nicholaus George Ngassa, Mbunge wa Igunga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kwamba nyumba za makazi ya askari Kituo cha Polisi Wilaya ya Igunga ambazo ni nyumba nne zenye kuishi familia 20 zimechakaa. Tathmini kwa ajili ya kubaini kiwango cha uchakavu na gharama za ukarabati imefanyika na kubaini kuwa kiasi cha shilingi 165,000,000.00 zitahitajika. Serikali imepanga kuanza kufanya ukarabati wa vituo na makazi chakavu ya askari wa jeshi la polisi, yakiwemo ya kituo cha polisi Wilaya ya Igunga kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante sana. (Makofi)