Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kuhamisha Gereza la Mkoa wa Iringa ili kuondoa muingiliano uliopo kati ya Gereza hilo na Hospitali ya Mkoa wa Iringa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na nishukuru sana majibu ya Naibu Waziri japokuwa yamekuwa ni hayo hayo muda mrefu.

Mheshimiwa Spika, changamoto iliyopo katika muingiliano huu wa hospitali na magereza kwa kweli unatesa sana wananchi wa Mkoa wa Iringa. Kiasi kwamba barabara ile imefungwa ambayo inaingilia hospitali kuna wakati wafungwa wakitolewa, ambulance inashindwa kupita inazunguka mzunguko mrefu sana kumuwahisha mgonjwa hospitali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kwa kuwa tulipokaa katika kikao cha Mkoa - RCC iliazimia kwamba kwa sababu hii changamoto haitatuliki basi tuiombe Serikali either ibadilishe kwamba majengo yaliyopo katika hospitali hii yawe hospitali ya wilaya na eneo ambalo lipo Frelimo kwa sababu ni kubwa sana linaweza likajengewa hata nyumba za madaktari basi iwe ndio hospitali yajengwe majengo ya hospitali ya mkoa. (Makofi)

Je, sasa Mheshimiwa Waziri yupo tayari kushirikiana na Wizara ya Afya ili kuona changamoto hii iweze kuondoa tatizo lililopo katika Mkoa wetu wa Iringa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; sambamba na hilo kwa kuwa katika Mkoa wetu wa Iringa pia lipo Gereza Kihesa Mgagao, Wilaya ya Kilolo, hili eneo ni eneo ambalo walikaa wapigania uhuru wa South Africa - ANC lakini utaona wenzetu walipokaa…

SPIKA: Mheshimiwa Ritta uliza swali.

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ndio.

Mazimbwi, Dakawa wamejenga vituo vya maendeleo kama shule hospitali lakini eneo hili bado kuna Gereza…

SPIKA: Uliza swali Mheshimiwa Ritta.

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, je, Serikali sasa kwa sababu tulikuwa tumeomba pia hilo Gereza lihamishwe ili kijengwe hata Chuo cha VETA… (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Dkt. Kabati kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza Wizara yangu iko tayari kuwasiliana na Wizara ya TAMISEMI na Wizara ya Afya ili kuona uwezekano wa kuhamisha mojawapo ya huduma kutoka Hospitali ya Mkoa iwe Hospitali ya Wilaya halina tatizo kabisa.

Mheshimiwa Spika, lakini hili la pili nadhani halikukamilika swali lenyewe kwa hiyo, nashukuru sana. (Makofi/Kicheko)