Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 14 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 166 2022-02-18

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kuhamisha Gereza la Mkoa wa Iringa ili kuondoa muingiliano uliopo kati ya Gereza hilo na Hospitali ya Mkoa wa Iringa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ritta Enespher Kabati, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali bado ina mpango wa kuhamisha Gereza hilo kwani eneo kwa ajili ya kuhamishia Gereza hilo, lilishapatikana maeneo ya Mlolo na Mbunge anafahamu jambo hilo. Kwa kuanzia Jeshi la Magereza lilishafungua kambi ijulikanayo kwa jina la Kambi ya Mlolo. Katika kambi hii zimejengwa nyumba 20 za watumishi na mabweni manne, kwa kutumia bajeti kidogo iliyokuwa inatengwa na Serikali kupitia vyanzo vya ndani vya Jeshi.

Mheshimiwa Spika, changamoto kubwa iliyokuwepo ni ufinyu wa bajeti hali inayopelekea kushindwa kutekeleza mpango huu. Aidha, kwa sasa gharama za ujenzi wa Gereza hilo zimeshaanza kupitiwa upya ili ziweze kuwekwa katika Mpango wa Maendeleo kwa bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023.

Mheshimiwa Spika, Serikali inapenda kutoa pongezi nyingi kwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa juhudi zake kupitia Mkuu wa Magereza wa Mkoa ambapo amekuwa mstari wa mbele kufuatilia maendeleo ya mpango huu. Aidha, natoa rai kwa wadau mbalimbali wa maendeleo waweze kujitokeza kuunga mkono juhudi za Serikali katika utekelezaji wa mpango huu. Nashukuru. (Makofi)