Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, tangu kuanzishwa kwa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, kuna changamoto gani katika kukuza na kuendeleza Mfuko wa Elimu ya Bodi ya Mikopo ili kukopesha wanafunzi wengi zaidi?

Supplementary Question 1

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kunipa nafasi, lakini pia niipongeze sana Serikali ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuongeza fedha nyingi sana kwa wasomi wa elimu ya juu. Kwa taarifa tu ni kwamba kati ya uamuzi mkubwa na wa kihistoria uliofanywa mwaka jana na Serikali, ilikuwa ni kusitisha tozo ya asilimia sita na riba ya asilimia 10 kwenye mikopo ya elimu ya juu jambo hili lilikuwa ni ni jambo la kheri sana.

Mheshimiwa Spika, ninayo maswali mawili ya nyongeza swali la kwanza; kwa kuwa Serikali ilisitisha fine ya asilimia sita na riba ya asilimia 10, lakini imesitisha kwa kutoa tamko ndani ya Bunge lako na sheria haijafutwa. (Makofi)

Je, Serikali haioni haja sasa ya kuleta hii sheria Bungeni, ili iweze kufutwa kabisa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili; kwa kuwa baada ya tamko hili la Serikali la kusitisha fine na riba ya asilimia sita na asilimia 10, watu wengi wamejitokeza kwenda kulipa fedha kwenye Bodi ya Mikopo. Lakini wamekuwa wakisumbuliwa kwamba walipe na madeni ya nyuma kabla ya tamko hilo la Serikali.

Ninaomba kauli ya Serikali kusitishwa kwa ulipaji wa riba ya asilimia sita na fine ya asilimia 10, inahusu madeni ya kuanzia lini kwa wananchi wa Tanzania? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Swalle, Mbunge wa Lupembe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mbunge kwa kuwapigania Watanzania wote, lakini vilevile tupokee shukurani zake kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuona changamoto ya tozo hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye eneo la kwanza la sheria nimtoe hofu Mbunge na Bunge lako Tukufu pamoja na kwamba Sheria ile bado haijaletwa hapa Bungeni, lakini bado utendaji wake haulazimishi uwepo wa tozo zile. Kwa hiyo, hata kama haitakuja bado katika utendaji wetu kwa sababu kanuni ndio ambayo inampelekea Mheshimiwa Waziri aweze kuweka kiwango gani cha tozo hizo za kulipwa. Kwa hiyo, nimtoe wasiwasi tunakwenda kufanya tathmini ya kina kwenye eneo hilo la sheria, kama tukiona kuna haja ya kuzileta hapa Bungeni tutaweza kuzileta kwa ajili ya marekebisho. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini eneo la pili ni eneo la madeni; ninaomba nimhakikishie Mbunge baada ya kauli ile ya kuondoa tozo zile pale pale makato yale yote kwa yule ambaye atakayekuwa hajalipa, hakupaswa kulipa tena na wale ambao wanaokuja baadae nao vilevile hawakupaswa kulipa. Kwa hiyo, kwa namna yoyote ile kama kuna mtu anaona kwamba anadaiwa hayo madeni ya nyuma basi tupate taarifa zake ili tuweze kuzifanyia kazi, lakini kwa mujibu wa sheria pamoja na tamko lile siku ile ile tulipozungumza hapa Bungeni makato yale na madeni yale yali-seize automatically. Ahsante sana. (Makofi)