Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufufua Kiwanda cha Tembo Chipboard kilichopo Kata ya Mkumbara Wilayani Korogwe?

Supplementary Question 1

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana; pamoja na majibu ambayo nina uhakika hayatawafurahisha wala kuwaridhisha watu wa Korogwe naomba kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, jambo la kwanza, jambo hili ni la muda mrefu sana na muwekezaji huyu hana uwekezaji wowote ambao ameufanya kwenye eneo lile, wapo wafanyakazi wa zamani wanadai, lakini pia wapo wawekezaji wengi wanajitokeza wanakitaka kiwanda hiki.

Nataka Serikali iniambie ni lini sasa zoezi la kurudisha kiwanda hiki rasmi itakamilika ili kuwezesha uwekezaji mwingine?

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili; kwa kuwa kuna malalamiko ya madai waliokuwa wafanyakazi kwenye eneo lile na kiwanda hiki ni muhimu kwa uchumi kwa watu Korogwe. Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari baada ya Bunge hili, Wizara ya Viwanda inayosimamia Sera, Ofisi ya Msajili wa Hazina na watu wa Maliasili waliokuwa wanakisimamia kiwanda hiki, tufanye ziara kwenda Korogwe tukazungumze kule namna nzuri ya kukikwamua kiwanda hiki kiweze kuwasaidia watu wa Korogwe? Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Thimotheo Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Thimotheo Mnzava kwa vile ambavyo anafuatilia sana maendeleo ya jimbo lake hususan katika sekta ya viwanda.

Mheshimiwa Spika, ni kweli jambo hili limekuwa la muda mrefu kama alivyosema tangu mwaka 2018 na kimsingi kama unavyojua kwa viwanda vyote ambavyo vilikuwa vimebinafsishwa kulikuwa na mikataba ambayo lazima Serikali iwe na uhakika inavyofanya urejeshwaji wake ili kusiwe na matatizo mengine ya kuingia utata kati ya wawekezaji hawa. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba taratibu za kisheria zikikamilika mapema iwezekavyo uwekezaji mpya katika kiwanda hiki utafanyika.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la lake pili, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge sisi kama Wizara ya Viwanda na Biashara, Serikali ina nia ya dhati kuhakikisha tunakwamua au tunaendeleza sekta ya viwanda. Tutaambatana baada ya Bunge hili tutawasiliana ili tuweze kufanya ziara na kuongea na wananchi wa Korogwe Vijijini ili tuone namna gani ya kusaidia kufufua kiwanda hiki muhimu kwa ajili ya maendeleo ya Jimbo la Korogwe Vijijini. Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufufua Kiwanda cha Tembo Chipboard kilichopo Kata ya Mkumbara Wilayani Korogwe?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi hii.

Mheshimiwa Spika, kiwanda kinachotajwa hapo malighafi yake inatoka katika Shamba la Misitu Shume ambayo ipo Lushoto na ninavyo fahamu mimi kiwanda hiki kwa sasa Msajili wa Hazina amekikodisha kwa mwekezaji mdogo wa pale Korogwe.

Je, kwa nini wasiboreshe mkataba ulipo sana na mwekezaji huyu mdogo ili angalau kuweza kuwasaidia wananchi wa Korogwe na Lushoto kwa ujumla?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika nakushukuru sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Rashid Shangazi, Mbunge wa Mlalo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali wakati inaangalia namna ya kuweza kukifufua kiwanda hiki ilikodisha kwa mwekezaji anayezalisha nguzo ambazo kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge zinatoka Lushoto.

Kwanza nia ni kuona kile kiwanda hakiharibiki kwa maana miundombinu ile iweze kuendelea kuwa bora. Lakini kama nilivyosema kwa sababu bado hatujamaliza mchakato wa kukirudisha rasmi Serikalini kwa hiyo hatuwezi kumpa mwekezaji mwingine mpaka tukamilishe taratibu za kisheria ili tusiwe na migogoro mingine na wawekezaji ambao wataingia katika kiwanda hivho. Nakushukuru sana. (Makofi)